• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Hospitali ya Wilaya Dodoma kujengwa

Imewekwa tarehe: July 5th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WILAYA ya Dodoma imemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia fedha shilingi 500,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya ili kusogeza huduma bora za afya karibu na wananchi.

Pongezi hizo zilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri wakati wa ziara ya Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma ilipotembelea na kukagua ujenzi wa Kituo cha Afya Chang’ombe.

Shekimweri alisema “hapa Dodoma hatuna hospitali ya wilaya, nichukue nafasi hii kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia fedha shilingi 500,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya pale Nala. Hatujaanza ujenzi sababu tumeomba idhini ya kujenga hospitali ya ghorofa. Nimshukuru Mganga Mkuu wa Jiji, Dkt. Andrew Method pamoja na wenzake hasa katika mazingira haya ambayo hatuna hospitali ya wilaya, Kituo cha Afya Makole kinafanya kazi kubwa kutusaidia kwa matibabu ya wagonjwa wa ndani”.

Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa wameshapokea watumishi wa Afya 18. “Namshukuru sana Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia watumishi wapya. Katika kituo hiki wameshapangwa watumishi 12, kwa hiyo, Mheshimiwa Diwani lile ombi lako kituo cha Afya kinakamilika hakina watumishi Rais Samia keshalijibu. Naomba muwapokee vizuri kama ulivyo mkarimu na wenzako muwapokee na kukaa nao kwa wema” alisema Shekimweri.

Akiwasilisha maelezo ya mradi huo, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt Andrew Method alisema kuwa mradi huo unatekelezwa kwa awamu mbili. “Awamu ya kwanza tulipokea shilingi 250,000,000 zilizojenga jengo la wagonjwa wa nje, maabara na kichomea taka. Kazi imekamilika kwa 99%. Awamu ya pili tumepokea shilingi 250,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la kina mama, jengo la upasuaji na jengo la kufulia. Ujenzi umeanza, tupo katika hatua ya msingi” alisema Dkt. Method.

Alisema kuwa ujenzi huo ukikamilika utahuduma wananchi karibu 30,000 waliokuwa wakizifuata huduma za afya Kituo cha Afya Makole. Alisema kuwa kituo cha Afya Makole kimekuwa na msongamano mkubwa wa wananchi wanaoenda kupata huduma hapo. “Tunatarajia kuanza kutoa huduma mwishoni mwa mwezi huu tarehe 29 baada ya kukamilisha uwekaji wa vifaa tiba na samani katika kituo hiko” alisema Dkt. Method.

Ujenzi wa Kituo cha Afya Chang’ombe ulianza tarehe 24 Desemba, 2021 kwa fedha za tozo kutoka serikali kuu.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.