• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Huduma ya maji Jijini yaendelea kuboreshwa

Imewekwa tarehe: January 14th, 2021

MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Dodoma (DUWASA) imesema katika kuhakikisha kuwa huduma ya maji inaboreshwa na kuwafikia watu wote jijini humo, inachimba visima kumi katika maeneo mbalimbali ya jiji lengo likiwa ni kukabiliana na kasi ya ongezeko kubwa la watu inayopelekea mahitaji makubwa ya huduma ya maji.

Kauli hiyo  imetolewa leo  na Mkuu wa kitendo cha Mawasiliano wa Mamlaka hiyo  Sebastian Warioba wakati akizungumza na Mtandao wa Dodoma News Blog Ofisini  kwake kuhusiana na Mikakati waliyoipaganga ya kuboresha huduma ya Maji katika jiji la Dodoma.

"Mpaka sasa ninavyozungumza kuna visima kumi vinavyochimbwa, tulianza kuchimba Zuzu na sasa tunachimba eneo la Ihumwa ambapo tumefanikiwa sana, tumepata visima vyenye maji ili tuweze kuhudumia eneo lile na katika eneo la Ntyuka tunataka kufanya vivyo hivyo lakini kwa upande wa Ihumwa tunataka tukichimba tunaweka na pampu na mabomba ili maji yaende kwenye tanki ambalo liko Njedengwa kwenye ukanda wa uwekezaji’’ alisema Warioba.

Wakati huo huo Warioba alisema kuwa, visima vingine kumi vitachimbwa kwenye maeneo mbalimbali katikati ya mji lengo likiwa ni kuongeza kiasi cha maji kwenye mitandao ili wanapotoa maji kwenye chanzo cha Mzakwe yawe yanakuta maeneo hayo ya mtandao yana maji.

"Zaidi ya hapo tumeshirikiana na wenzetu wa mabonde wa Wizara ya Maji na tumeainisha visima vya miaka ya nyuma kama utakumbuka juzi tulikuwa na ziara ya Naibu katibu Mkuu wa Wizara hiyo tulitembelea moja ya visima kama hivyo kiko pale Nzuguni...visima vile vilichimbwa miaka ya nyuma na mpaka sasa tunapozungumza tumeshaainisha visima kumi na tatu vilivyochimbwa miaka hiyo na Serikali, wakati huo kulikuwa na shida ya maji katika mji wa Dodoma lakini baada ya kupata maji ya kutosha visima vile vilikuwa havitumiki kwahiyo tunachokifanya sasa tumevitambau na tumeanza na kile cha Nzuguni na vingine tumeweka wataalamu ambao wanavisafisha kwa maana ya kukarabati na kupima kiasi cha maji yanayotoka mle na ubora wake halafu baadaye tunafunga pampu’’ alifafanua Warioba.

Aliongeza kuwa, Mamlaka hiyo pia imeanzisha magrupu ya mtandao wa kijamii wa 'Whatsapp' kwa ajili ya kupata taarifa mapema ambazo zimekuwa zikijitokeza kwenye maeneo mbalimbali.

"Tuna magrupu kama matatu, magrupu ya 'whatsapp' yapo mawili na moja la 'Telegaram' ambapo tuna watu wengi wamejiunga, lengo letu ni kurahisisha utaratibu wa mawasiliano kati yetu sisi DUWASA na wadau na mwitiko ni mkubwa na tumekuwa tukitoa taarifa mbalimbali kupitia magrupu hayo" aliongeza.

Hata hivyo, alitoa wito kwa wale ambao wamekuwa wakitumia maji kinyume na sheria kuacha mara moja na kwa atakayebainika kufanya hivyo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.