• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Idara ya Ardhi kupiga kambi Michese kumaliza migogoro

Imewekwa tarehe: February 3rd, 2021

IDARA ya Ardhi, Mipango miji na Maliasili katika Jiji la Dodoma itahamia eneo la Micheze lililopo Kata ya Mkonze kwa siku 14 kusikiliza na kutatua kero za wananchi zinazohusu ardhi kwa lengo la kuwasogezea huduma na kuwaharakishia maendeleo wananchi.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru alipokuwa akiongea na wananchi wa eneo la Michese lililopo Kata ya Mkonze kwenye mkutano wa hadhara jijini hapa jana.

Mafuru alisema kuwa aliamua kwenda kufanya mkutano wa hadhara na wananchi wa Michese kutokana na kupokea barua nyingi zinazolalamikia upimaji na changamoto zake. “Maelekezo ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Magufuli ni kwamba viongozi tutoke ofisini na kuwafuata wananchi kuwasilikiza na kutatua kero zao. Nikiwa ofisini nimekuwa nikipokea barua nyingi kutoka Kata ya Mkonze, zikilalamikia juu ya upimaji na changamoto zake. Sasa kama kiongozi, wingi wa barua hizo za malalamiko unanipa picha kuwa kuna tatizo, ndiyo maana nimekuja hapa na timu yangu kuwasikiliza na kutatua changamoto hizo” alisema Mafuru.

Katika masaa yake matano ya kupokea, kusikiliza na kutatua kero za wananchi, mkurugenzi huyo aliiagiza Idara ya Ardhi, Mipango miji na Maliasili katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwenda na kuweka kambi katika eneo la Michese kusikiliza changamoto ya kila mwananchi na kuitatua. “Ndugu zangu, nitagawa timu ya wataalam wangu wa jiji, kampuni ya upimaji, timu ya urasimishaji na viongozi wa mitaa katika mitaa mitatu ya eneo la michese kuanzia Jumatatu. Watakaa hapa kwa siku 14 kupokea na kusikiliza kila mwananchi lalamiko lake na kulipatia ufumbuzi. Malalamiko yatakayohitaji kwenda ‘site’ wataenda” alisema Mafuru.

Aidha, aliitaka kampuni inayofanya zoezi la upimaji kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria na kwa uwazi ili kuwatendea haki wananchi. “Naiagiza kampuni inayofanya zoezi la upimaji kubandika ramani zote za utambuzi katika mbao za matangazo kwenye ofisi za mitaa yote zoezi lilipotekelezwa ili kila mwananchi aone na kumtambua jirani yake. Vilevile, bandikeni ramani za Mipango miji. Ramani hizi zikibandikwa na maelezo yake kutolewa kwa uwazi zitaondoa lugha ya ubabaishaji na kuonesha uwajibikaji na hatimae kuondoa malalamiko” alisisitiza Mkurugenzi Mafuru.

Kwa upande wake, mkuu wa Idara ya Ardhi, Mipango miji na Maliasili, Amelye Chaula alisema kuwa hakuna kiwanja kitakachouzwa kinyemela katika eneo hilo. “Ndugu zangu, niwatoe hofu, hivi viwanja baada ya kukamilika ramani ndio zoezi la ugawaji litaanza rasmi. Mmemsikia Mkurugenzi wa Jiji maelekezo aliyotoa, lazima ramani zote zibandikwe na kila hatua ifanyike kwa uwazi. Hivyo, kama kuna aina yoyote ya ugawaji ambayo imefanyika, imefutwa rasmi” alisema Chaula.

Naye Afisa Mipango miji katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Aisha Masanja alisema kuwa zoezi la upimaji shirikishi linalofanyika katika eneo la Michese linalenga kuboresha eneo hilo ili liwe linajitosheleza kihuduma. “Halmashauri tunataka kuwa na Michese inayojitosheleza kwa kuwa na huduma zote muhimu ili kuwaondolea kero wananchi kufuata huduma maeneo ya mbali. Tumesikia malalamiko ya wananchi juu ya umilikishaji ardhi. Napenda kuwahakikishia wananchi kuwa zoezi la umilikishaji ardhi litafanywa na halmashauri na siyo kampuni ya upimaji. Halmashauri ndiyo yenye mamkala kisheria kumilikisha ardhi. Hivyo, hakuna ardhi itakayomilikishwa na kampuni ya upimaji” alisema Masanja kwa kujiamini.

Kata ya Mkonze ina jumla ya mitaa nane ambayo ni Chidachi, Miganga, Chinyika, Chisichiri, Muungano A, Muungano B, Bwawani na Nzinje.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.