• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Igeni Jiji la Dodoma kukusanya; kujenga vitega uchumi kwa mapato ya ndani - Waziri Mkuu

Imewekwa tarehe: July 24th, 2019

MAMLAKA za Serikali za Mitaa nchini zimetakiwa kuiga mfano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kujenga majengo ya vitega uchumi ili ziweze kujitegemea.

Kauli hiyo ilitolewa na Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa (Mb) alipokuwa akifungua mkutano mkuu wa Jumuiya ya Serikali za mitaa (ALAT) kwa niaba ya Rais Dkt John Magufuli jijini Mwanza jana.

Majaliwa alisema kuwa Mamlaka za Serikali za mitaa zinakusanya fedha lakini haziendi kwenye miradi ya maendeleo. Hivyo, alizitaka kutenga asilimia 40 ya mapato yake kwa ajili ya shughuli za maendeleo. “Kuna Halmashauri nyingi zinafanya vizuri kwenye makusanyo lakini fedha hazijulikani zinaenda wapi, Dare s Salaam, Arusha ni baadhi ya zinazokusanya fedha lakini hamna mradi hata mmoja. Ukichukulia Dar es Salaam au Arusha ambao wanakusanya kati ya shilingi Bilioni tano na 10, ni mradi gani wa thamani kubwa uliojengwa kwa kutumia fedha zenu za ndani, ukiacha hii mikubwa ya stendi ya mabasi au barabara za lami ambayo inajengwa kwa fedha za serikali kuu?” alihoji Majaliwa.

Alizitaka Halmashauri hizo kuiga mfano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma inayojenga majengo ya biashara kwa mapato ya ndani. “Afadhali hawa wa Dodoma ambao wanajenga stendi ya mabasi na hoteli mbili za kitega uchumi” alisema Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa.

Aidha, alizitaka Halmashauri kujenga miradi mikubwa inayogusa maisha ya wananchi moja kwa moja. Hasa ikizingatiwa kuwa Halmashauri zina jukumu kubwa la kutoa huduma za kwa wananchi walio katika maeneo yao ya kiutawala.

Mkutano wa ALAT unafanyika jijini Mwanza kwa siku tatu ukihudhuriwa na washiriki zaidi ya 600 wakiwemo Mameya wa Majiji na Manispaa, Wenyeviti wa Halmashauri za Miji na Wilaya na Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za mitaa.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.