• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Indonesia yajipanga kuhamishia ubalozi Dodoma

Imewekwa tarehe: September 19th, 2023

BALOZI wa Indonesia nchini Tanzania Bw. Tri Yogo Jatmiko pamoja na ujumbe wake, wamemtembelea Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ofisini kwake leo Septemba 19 kuzungumza kuhusu utaratibu wa kuhamishia ofisi za Ubalozi huo kwenye Mji Mkuu wa Serikali Dodoma kwa lengo la kutekeleza agizo la Serikali la kuhamishia Makao Makuu ya nchi Mkoani Dodoma na kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Katika mazungumzo yao Balozi Jatmiko amesema mwezi uliopita Rais wa Indonesia alikuja Tanzania na kuonana na Mhe. Rais Samia ambapo moja ya mambo waliyozungumza lilikua ni swali kutoka kwa Mhe. Rais Samia kuhusu lini Ubalozi wao utahamia Dodoma. Kufuatia mazungumzo ya viongozi hao, Mhe. Balozi ameamua kufunga safari hadi kwenye ofisi hii ili kupata utaratibu wa ujenzi wa ofisi za Ubalozi kutoka kwa mwenyeji wao Mhe. Senyamule.

Akitoa ufafanuzi juu ya eneo lililotengwa kwa ajili ya Mabalozi wa nchi mbalimbali katika Mji wa Serikali Mtumba, Mratibu wa Mradi wa ujenzi wa Mji wa Serikali Dodoma Bw. Meshack Bandawe, amesema kuwa Balozi zote zilizopo nchini zimetengewa maeneo maalumu na yenye ukubwa unaolingana wa heka 2.5 kwa eneo la ofisi na pia kuna maeneo kwa ajili ya makazi na watumishi wa Balozi hizo. Amewaonyesha ramani ya eneo lao ikiwemo majirani waliopakana nao ambao ni Ubalozi wa Burundi, Algeria, Namibia pamoja na Vietnam. Hata hivyo, amebainisha kuwa ujenzi wa Mji wa Serikali kwa sasa umefikia asilimia 70 hadi 80.

Mkuu wa Mkoa Mhe. Senyamule, ameupongeza Ubalozi huo kwa kufuatia taratibu za ujenzi wa ofisi za Ubalozi na kuhamia Dodoma kwakuwa ni wakati sahihi kwao kulingana na miradi mbalimbali ya maendeleo inayoendelea kujengwa Dodoma ikiwemo uwanja wa ndege wa Msalato ambao utarahisisha shughuli za safari za kuingia na kutoka Dodoma. Pia amezungumzia ujenzi reli ya kisasa ya SGR ni miradi mingine ya kimkakati itakayorahisisha shughuli za kibalozi zitakapokua ndani ya Mkoa wa Dodoma.

Balozi Jitmiko amesisitiza kupatiwa nyaraka zitakazohusiana na eneo lao ili aweze kuziwasilisha kwa Waziri wao na kujadiliwa kwenye Bunge la Indonesia kwa ajili ya kupangwa bajeti ya ujenzi ili uweze kuanza mara moja. Pia Balozi huyo amesema Indonesia ipo tayari kushirikiana na Tanzania kwenye maeneo mbalimbali ya kiteknolojia ikiwemo kwenye sekta za madini na umeme kwani huko kwao wana teknolojia za kisasa.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule (kulia) akimkaribisha mgeni wake Balozi wa Indonesia nchini Tanzania Bwana Tri Yogo Jatmiko ofisini kwake jengo la Mkapa jijini Dodoma leo.

Balozi wa Indonesia nchini Tanzania Bwana Tri Yogo Jatmiko (wa kwanza kulia) akiwa ameambatana na ujumbe wake akiweka saini kitabu cha wageni kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma.

Mratibu wa Mradi wa Ujenzi wa Mji wa Serikali Dodoma Bwana Meshack Bandawe (aliyesimama) akiwaonesha Balozi wa Indonesia nchini na ujumbe wake ramani ya eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za Mabalozi kwenye Mji wa Serikali Mtumba.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.