• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jafo aelekeza Halmashauri kukarabati samani za shule

Imewekwa tarehe: February 28th, 2020

Serikali imeziagiza halmashauri zote nchini kukarabati samani za shule kupitia fedha zinazopelekwa shuleni za program ya Elimu Bila Malipo ili kuondoa tatizo la madawati kwenye shule nchini.

Kauli hiyo iliitoa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Selemani Jafo tarehe 20/02/20202 wakati akipokea taarifa ya tafiti iliyofanya kati ya Chuo Kikuu cha Dodoma na taasisi ya Mdigri Logistics kuhusu vifaa vya Ufundishaji na Ujifunzaji kwenye shule za sekondari. Tafiti hiyo imefanyika katika mkoa wa Dodoma na hafla ya kukabidhi taarifa ilifanyika katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa Dodoma.

“nielekeze Mamlaka za Serikali za Mitaa katika Halmashauri zote kwa Wakurugenzi, kupitia na kushughulikia madawati na meza zote na kuhakikisha zinakarabatiwa kupitia fedha za Elimu Bila Malipo”

Jafo amezitaka Mamlaka za Serikali za Mitaa kutumia vikundi vya vijana kufanya ukarabati wa miundombinu ya madarasa, madawati na vifaa vingine vya shule ikiwa ni sehemu ya kuwapa ajira vijana na kuboresha mazingira ya elimu katika shule zilizopo kwenye mamlaka zao badala ya kusubiri kutenga fedha kutengeneza madawati mapya.

“Halmashauri zitumie vikundi vya vijana kufanya uakarabati wa miundombinu ya madarasa, madawati na vifaa vilivyopo katika shule, haiwezekani kusubiri kutenga fedha za  madawati mapya wakati yapo madawati ya zamani na hayajakarabatiwa” alisema Waziri Jafo.

Vilevile, Waziri Jafo amesema pamoja na watendaji hao kukarabati samani za shule pia wakarabati miundombinu ya shule yakiwemo majengo, matundu ya vyoo, madarasa na miundombinu mingine kwenye sekta ya elimu iweze kudumu na kutumika kwa muda mrefu.

Aidha amewataka Wakuu wa shule kuendelea kusimamia masuala ya kitaaluma, mazingira na miundombinu kama kipaumbele chao na kuboresha hali ya taaluma nchini.

Jafo amewataka watafiti hao na wengine kuendelea kufanya tafiti kwenye sekta ya elimu na kuyapa kipaumbele maeneo mengine kama miundombinu ya vyoo, madarasa na vinakilishi ili kutoa mchango wa kufanya maboresho kwenye elimu ya msingi.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Satano Mahenge amesema watafiti wamefanya tafiti na kubaini tunalo tatizo katika eneo la elimu na kwamba watanzania hatuna utamaduni wa kukarabati madawati na miundombinu hivyo tafiti itatusaidia kuboresha miundombinu kwenye sekta ya elimu.

Awali Dkt. Ombeni Msuya kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma aliwasilisha taarifa ya tafiti ya vifaa vya Ufundishaji na Ujifunzaji kwenye shule za sekondari 35 na kusema kuwa utafiti huo umefanyika kwenye Halmashauri 7 zote za mkoa wa Dodoma kuanzia mwezi Januari, 2019 hadi januari, 2020 na kubaini changamoto kadhaa ikiwemo kutokuwepo kwa zana za kufundishia zinazokidhi mahitaji, kuwepo kwa viti, meza na vifaa vya maabara visivyo na ubora, kuwepo kwa meza 91,000 na viti 915 ambavyo havitumiki na vinahitaji ukarabati mdogo.

Dkt. Msuya ametoa rai kwa Serikali kuundwa kwa kikundi kazi kitakachokuwa kinakarabati samani na miundombinu ya shule ‘Maintainance Mobile Unit’ ambao wanaweza kutoka katika vyuo vya ufundi ili kuendelea kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia shuleni.

Kwa upande wake Yoram Mkwawa Mkuu wa shule Mbabala ametoa rai ya kuendelea kuwaelimisha wananchi kuhusu Sera ya Elimu Bila Malipo kwani kuna upotoshwaji mkubwa kuhusu sera hiyo ambapo wazazi wengine hawapo tayari kuchangia chochote kwa ajili ya maendeleo ya shule zao lakini pia amewataka Wakuu wa shule kuwa wabunifu katika kukabiliana na changamoto mbalimbali shuleni badala ya kusubiri fedha kutoka Serikalini.

Chanzo: Tovuti ya tamisemi.go.tz


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.