• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jafo:Mikopo ya Halmashauri kwa vikundi sasa kwa watu watano, mmoja

Imewekwa tarehe: March 2nd, 2021

SERIKALI imefanya mabadiliko katika muundo wa kanuni za mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri ambapo kwa sasa katika kundi la vijana na wamama kikundi kinaweza kupokea mkopo kuanzia watu watano na kwa walemavu hata mtu mmoja anaweza kupokea mkopo.

Hayo yamebainishwa jijini Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo wakati akifunga mkutano wa siku tatu wa mwaka wa chama cha wataalamu wa Maendeleo ya Jamii uliofanyika kwa siku tatu jijini Dodoma.

Amesema alipokea maombi mengi kuhusu kanuni inayotaka kikundi lazima kuwa na watu kuanzia kumi kuwa baadhi ya maeneo imekuwa changamoto kuwapata watu wanaokubaliana na kuwa Pamoja na kutembea Pamoja.

“Katika maeneo mengi ni vigumu sana kuwapata watu wanaokubaliana kuwa Pamoja hadi kufikia kumi, na hasa kwa walemavu imekuwa ngumu kuwapata kumi wenye ulemavu wa aina moja, sasa hata mtu mmoja mwenye ulemavu anaweza kukopa” amesema Mhe. Jafo.

Amesema kuanzia sasa maafisa maendeleo ya jamii watapata nakala za kanuni mpya zitakazo kwenda kuwaongoza katika kutekeleza majukumu yao katika maeneo yao ya kazi kundi la vijana na kundi la akina mama hata wakikubaliana wakifikia watano wataruhusiwa kupata mikopo hiyo.

Aidha amebainisha kuwa wamefanya marekebisho hata katika kuhakikisha urejeshwaji wa mikopo hiyo unaimarika sasa watatenga fedha kwa ajili ya ufuatiliaji wa mikopo, halmashauri zimetengwa  katika makundi ambapo halmashauri zenye mapato yasiyozidi bilioni moja lazima watenge kila mwezi kiasi cha laki tano hadi milioni moja.

Wakati katika halmashauri zenye mapato kuanzia bilioni 1 hadi bilioni 2 wao watatenga kiasi cha shilingi milioni moja hadi milioni moja na nusu, na kwa halmashauri zinazokusanya kuanzia bilioni 5 na kuendelea lazima watenge kiasi cha shilingi milioni 5 kila mwezi kwa ajili ya kuwawezesha maafisa maendeleo ya jamii kuvifuatilia hivyo vikundi.

“Nasisitiza fedha hizi ni kwa ajili ya marejesho ya mikopo na sio fedha zilizotengwa kwahiyo kama hufuatilii vikundi hivyo au hakuna marejesho ya vikundi fedha hizi zisitengwe, tunafanya hivi ili ufuatiliaji uimarishwe” amesema.

Amesema kwa miezi sita tayari serikali imetumia kiasi cha shilingi bilioni 24, na kwa kipindi cha miaka mitano serikali imetumia kiasi cha shilingi bilioni 143 kutoa kwa vikundi vya akina mama, vijana na watu wenye ulemavu kote nchini.

Amewashukuru wataalamu wa maendeleo ya jamii kwa kazi kubwa wanayoendelea kufanya hapa nchini na kubainisha kuwa kwa sasa kitengo hicho kinazidi kuimarika tofauti na hapo mwanzo ambapo kilikuwa kikidharaulika sana.

Amesema katika maeneo yao ya kazi kuna miradi mingi ya maendeleo inayotekelezwa hivyo ni wajibu wao kuhakikisha wanatoa elimu kwa jamii umuhimu wa miradi hiyo na itakavyowanufaisha wananchi wenyewe ili wailinde kikamilifu.

Amewataka kutumia mafunzo waliyoyapata kupitia mkutano huo kwenda kufanya kazi kwa ufanisi ukubwa ili taifa kupata tija kwa sababu wao ndio kiungo muhimu katika maendeleo ya yananchi katika maeneo hayo hivyo wahamasishe wananchi katika kujipatia maendeleo yao.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii Patrick Golwike amesema wataalamu hao wamekutana kwa siku tatu kwa lengo la kujadili namna ya kuboresha taalamu hiyo katika maeneo yao ya kazi.

Amesema kwa sasa wameboresha mkutano huo, kwani awali walikuwa wakihudhuria wakuu wa idara pekee lakini kwa sasa wanashirikisha wataalaumu wote hadi ngazi za chini kabisa ili kuboresha taaluma, na kwa mwaka huu wamewakutanisha na watunga sera ili elimu hiyo iwefikie kwani wao ndio watekelezaji wa sera hiyo.

Katika mkutano huo umetumika katika kuchagua viongozi wapya watakaoongoza  wataalamu wa chama kwa kipindi kingine ambapo nafasi ya mwenyekiti ameshinda Bi Angela Mvaa, Makamu mwenyekiti Dkt Regina Malima na kiti cha katibu Mkuu ni Daniel Wambura.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.