• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jamii imeaswa isifumbie macho Ukatili wa Kijinsia

Imewekwa tarehe: December 6th, 2024


Na. Faraja Mbise, DODOMA

Jamii imeaswa kutoyafumbia macho masuala ya ukatili wa kijinsia na kutakiwa kuripoti kwenye vyombo vya sheria matukio ya ubakaji, ulawiti na ndoa za utotoni.

Hayo, yalisemwa na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ng’hongh’onha, Patrick Mwachambi ambaye ni muwakilishi wa mgeni rasmi, alipokuwa akizungumza na wananchi waliojitokeza katika Uzinduzi wa Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia ngazi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika Kata ya Ng’hong’onha.“Natoa wito kwa wananchi wenzangu, kuwatumia ipasavyo wataalam wetu kwasababu wako tayari wakati wote kuhakikisha kuwa vitendo vya ukatili vinakomeshwa na wahusika wanachukuliwa hatua za kisheria. Namshukuru sana Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, tumejifunza mengi kupitia wataalam. Kwahiyo, nawaomba wananchi tuzingatie elimu tuliyopewa na kuahidi kuifanyia kazi, yote yaliyoelekezwa tutayatekeleza bila kuathiri taratibu za kisheria” alisisitiza Mwachambi.

Akizungumzia kampeni ya mwaka huu isemayo “Kuelekea miaka 30 ya Beijing: CHAGUA Kutokomeza Ukatili wa Kijinsia” mgeni rasmi alitoa historia fupi kuhusiana na harakati za kupambana na kutokomeza ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto.

“Kaulimbiu hii inaendelea kusisitiza kuendeleza mapambano dhidi ya ukatili yaliyoanza miaka mingi nyuma na kutiliwa mkazo na Mkutano wa Beijing wa mwaka 1995 ambao ni mkutuno wanne wa Dunia kwa wanawake uliofanyika Beijing nchini China. Mkutano huu uliwakutanisha kwa pamoja serikali za mataifa mbalimbali pamoja na wanaharakati, na uliwezesha kuundwa kwa jukwaa la kuchukua hatua la Beijing, na agenda ya msingi ya haki za wanawake katika ngazi za kimataifa ambao kati ya malengo yake makubwa ni kutokomeza ukatili wa kijinsia na kusisitiza upatikanaji wa haki za wanawake katika nyanja zote za kimataifa na kutetea haki za kijinsia” alisema Mwachambi.

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii ambae ni Mratibu wa Jinsia na Watoto Jiji la Dodoma, Fatuma Daudi, alizungumzia mlolongo wa matukio mbalimbali ambayo yanaadhimishwa ndani ya siku 16 za kupinga Ukatili wa Kijinsia. Daudi alisema “tukiwa tupo katika kampeni za siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, kampeni hizi zinatokana na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Kimataifa Kofi Annan ambaye aliona vitendo vya ukatili wa kijinsia unazidi  hivyo kitengwe kipindi maalum cha kufanya kampeni ili kukomesha vitendo vya ukatili wa kijinsia. Kipindi kilichaguliwa kuanza tarehe 25 Novemba na kuisha tarehe10 ya mwezi Desemba, ukizihesabu siku hizi zinafika siku 16, ndani ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kuna siku mbalimbali zenye matukio maalum kati ya hizo kuna siku ya Novemba 25, ambayo ni siku ya kupinga ukatili na unyanyasaji dhidi ya wanawake, Novemba 29, ambayo  ni siku ya kimataifa ya utetezi wa haki za wanawake, Desemba moja ambayo ni siku ya UKIMWI Duniani, Desemba 05, siku ya kujitolea Duniani na siku hizi zinahitimishwa na tarehe 10 Desemba, ambayo ni siku ya Kimataifa ya Haki za Binadamu. Siku hizi zote zipo ili kuhakikisha wanawake, watoto na Jamii kwa ujumla inaepukana na vitendo vya ukatili”.

Kuhusu msaada wa kisheria unaopatiwa kwa wahanga wa ukatili wa kijinsia, Afisa Maendeleo ya Jamii, Dawati la Msaada wa Kisheria katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Frida Ngowi aliogelea umuhimu wa dawati la sheria katika kupambana na masuala ya ukatili wa kijinsia.

“Dawati hili la msaada wa kisheria lipo kwa ajili ya kutoa elimu ili watu tufahamu haki zetu, pili dawati hili linawasaidia watu kupata huduma za msaada wa kisheria ambapo kuna makundi maalumu, kundi la kwanza ni wanawake, watoto, walemavu na wazee lakini pia mwananchi yeyote ambaye hana uwezo wa kumudu gharama za mahakama. Kwahiyo, huduma tunazotoa ni pamoja na ukatili wa kijinsia unaotendeka kwa wanawake, watoto na wanaume pia wanaopitia changamoto za ukatili wa kijinsia” alisisitiza Ngowi.

Vilevile, Afisa Ustawi wa Jamii Mwanadamizi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Aneth Mwambya aliwasisitiza watoto kutoa taarifa kwa wazazi, dawati la kijinsia au kwa walimu endapo watakutana na vitendo hivyo viovu vya ukatili wa kijinsia. “Ukatili wa ngono au kingoni, tunauona, tunaenda likizo, takwimu zinasema asilimia 60 ya ukatili unafanyika nyumbani, unapofanyiwa kitendo chochote ambacho si kwa ridhaa yako kwa maana unapata madhara kiakili, kimwili na kingono unatakiwa utoe taarifa kwa wazazi, jirani kama unamwamini, dawati la jinsia, kituo cha polisi na serikali za mitaa” alisisitiza Mwambya.

Nae Mwanafunzi wa Shule ya Msingi ya Ng’hong’onha, Theresia Samson alitoa rai kwa watoto wanaopitia ukatili wa kijinsia majumbani kwao, waweze kuripoti matukio hayo ili kupunguza idadi ya matukio ya ukatili wa kijinsia. “Mimi nimeigiza kama mtoto niliyebakwa na mjomba, nawashauri watoto wengine wanaofanyiwa vitendo hivi wasikae kimya wakatoe taarifa kwa walimu, watu wanaowaamini au kwa wazazi wao” alishauri Samson.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.