• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jamii yatakiwa kuondokana na mila kandamizi kwa wanawake

Imewekwa tarehe: March 8th, 2020

JAMII nchini imetakiwa kuondokana na mila potofu zinazomkandamiza mwanamke na kufanya kuonekana mnyonge, asiye na haki na dhaifu ili kuweza kumpa uwezo wa kuonyesha uwezo alionao kwani wanawake ni taifa kubwa.

Hayo yalisemwa na Katibu wa Chama cha Wanawake Tanzania katika Biashara (TWCC) Taifa, Amina Mpore wakati akisoma risala katika kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani machi 8 mwaka huu kwa mgeni rasmi Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Dodoma Felista Bura, ambapo aliainisha changamoto ambazo wanawake wamekuwa wakikumbana nazo.

Mpore alisema juhudi za kuwakomboa wanawake zinadidimizwa na jamii kwa kuwa bado wanaendelea kukumbatia mfumo dume katika nyanja muhimu na kumuachia mwanamke mzigo wa malezi ya familia bila kuwa na msaada wa aina yeyote kutokana na mila ambazo hazimruhusu mwanamke kutoa mchango wake.

“Bado wanawake wana kikwazo kikubwa kinachozuia maendeleo yao kuonekana katika jamii, mimba na ndoa za utotoni bado ni changamoto, mtoto wa kike anakabiliwa na changamoto hiyo kubwa, anakosa haki yake ya kimsingi, anakosa kuwa na haki ya kuchagua kipi anakihitaji kwa muda huo, badala yake mila zetu zinamlazimu kuzifuata kutokana na jamii kushindwa kukubaliana na mabadiliko ya kweli ya ulimwengu wa sasa.

“Wanawake bado wanakosa haki ya kurithi ardhi na kumiliki mali, unakuta mwanamke ana familia na mali zake lakini mara tu baada ya mume wake kufariki ananyang’anywa kila kitu  anarudishwa nyuma kimaendeleo, anaanza upya wakati alishapiga hatua, jambo hili linakatisha tamaa, linamdumaza mwanamke wa kitanzania na linamfanya anakata tamaa ya maisha”, alisema Katibu huyo.

Pia, alisisitiza suala la mabadiliko kwa jamii, ili kuweza kujenga kizazi imara na chenye mtazamo wa kimaendeleo kwa kuhakikisha wanawake wanapewa kipaumbele kwani kupitia wao jamii inaweza kujengwa vyema ikiwa yenye maadili ama la jamii itaharibika.

“Kauli mbiu ya mwaka huu inasema kizazi cha usawa kwa maendeleo ya Tanzania ya sasa na ya baadaye, kutokana na kaulimbiu hii jamii ipate mabadiliko ya kweli katika kutekeleza usawa wa kila jambo baina ya mwanamke na mwanaume, ili tuweze kuondokana na mfumo unaompa kipaumbele mwanaume kwa kila jambo.

“Kauli mbiu hii isiishie leo, ikaendelezwe katika jamii yetu tena kwa matendo, mtoto wa kike akaendelezwe kielimu, afanikishe ndoto zake, apewe stadi za maisha ili aweze kujikwamua, apewe na elimu kuhusiana na afya ya uzazi ili aweze kujitambua, tukiyazingatia haya tutatengeneza kizazi bora kijacho, tutawaachia urithi bora watoto wetu  tena wa elimu endelevu usiyoharibika”, alisema Mpore.

Risala hiyo ilihitimishwa kwa kuishauri jamii kuondokana na mila potofu, zinazomkandamiza mwanamke hususani ukeketaji pia, imeshauriwa mwanamke apatiwe fursa ya kupatiwa nafasi ya kuonyesha uwezo alionao ili jamii iweze kutambua na kuenzi nafasi yake, jamii, vyama vya siasa, Serikali na asasi za kiraia kutafakari kwa undani mafanikio na changamoto zinazowakabili wanawake katika kuleta maendeleo yao na ya jamii kwa ujumla.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.