• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Japan yaonesha nia kukisaidia Chuo Kikuu cha Dodoma

Imewekwa tarehe: August 27th, 2022

KAMPUNI ya Japan ya Association of African Economic Development (AFRECO) imeonesha nia ya kujenga chuo cha uhandisi wa tiba (school of medical engineering) kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ili kupunguza tatizo la wataalamu wa tiba na vifaatiba nchini.

Hayo yameelezwa na Rais wa kampuni hiyo, Bw. Tetsuro Yano jana jioni (Jumamosi, Agosti 27, 2022) alipokutana na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa jijini Tunis, Tunisia ambako anamwakilisha Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwenye Mkutano wa Nane wa Kimataifa wa Wakuu wa Nchi na Serikali unaohusu Maendeleo ya Japan na Afrika (TICAD8).

“Tumeona haja ya kuanzisha chuo cha uhandisi tiba ili tuweze kufundisha wataalamu watakaokuwa wakifanya matengenezo ya vifaa badala ya kuagiza mafundi kutoka nje, au kuviacha visitumike tena,” alisema.

Pia alimweleza Waziri Mkuu kwamba walishapokea maombi kutoka UDOM ya kupatiwa basi la kutoa tiba lenye vifaa mahsusi vya hospitali (mobile clinic bus) ambalo litakuwa likisaidia kutoa huduma kwenye vijiji vya jirani na chuo hicho.

Naye mtaalamu kutoka Chuo Kikuu cha Sayansi na Sanaa cha Kurashiki cha Japan, Dkt. Tomotaka Naramura alimweleza Waziri Mkuu kwamba wana nia ya kufungua chuo hicho mwaka 2023.

Alisema walikutana na Mkuu wa chuo hicho na wakakubaliana kuwa ipo haja ya kuendeleza rasilmali watu kwenye upande wa tiba ili kuwe na wataalamu mahsusi kwa ajili ya vifaa tiba vinavyonunuliwa.

Kwa upande wake, Waziri Mkuu aliwashukuru kwa kuonesha nia ya kuendeleza sekta ya afya na hasa kwenye eneo la vifaa tiba kwani linaendana na matarajio ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ya kutaka kuboresha afya za Watanzania kwa kuhimiza ujenzi wa hospitali, vituo vya afya na zahanati.

“Serikali ya Tanzania imeridhishwa na nia ya kampuni yenu ya kuwekeza kwenye uhandisi wa tiba kwani tunawahitaji sana watumishi wa hiyo kada. Hawa watasaidia siyo UDOM peke yake, bali Muhimbili, Bugando, KCMC na vituo vingi vya afya ambako Serikali ya awamu ya sita imepeleka vifaa tiba,” alisema.


Chanzo: Ukurasa rasmi wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Instagram)

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.