• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji Dodoma 'halikamatiki' kwa miradi ya maendeleo, Hotel ya ghorofa 11 kujengwa

Imewekwa tarehe: August 29th, 2019

MBUNGE wa Dodoma Mjini, Mhe. Antony Mavunde amesema ujenzi wa hoteli ya nyota nne katikati ya Jiji la Dodoma utachochea maendeleo, biashara na utoaji huduma za kijamii jijini hapo.

Amesema hayo kabla ya Mkurugenzi wa Jiji, Godwin Kunambi na Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma kusaini mikataba miwili ya kujenga hoteli ya nyota nne yenye ghorofa 11 na kitega uchumi  kwenye mji wa serikali eneo la Mtumba.

Mavunde ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira alisema ujenzi wa miundombinu ya hoteli na miradi mingine itaongeza chachu ya kuibadilisha Dodoma ambayo miaka iliyopita haikuwa hivi.

Alifafanua kuwa miaka 20 iliyopita Dodoma, mwisho kutembea magari na watu mjini ilikuwa saa mbili usiku, lakini sasa jiji limebadilika unaweza kukutana na watu na magari baada ya muda huo.

Alimpongeza Kunambi kwa ubunifu na ujenzi wa miundombinu, ikiwemo ya hoteli ya nyota nne katikati ya jiji hali inayochochea maendeleo ya jiji ambalo ni makao makuu ya serikali.

Mavunde alisema kuwepo kwa miundombinu ya hoteli kutachochea kukua kwa maendeleo na kuongeza biashara na wakulima wadogo kupata nafasi ya kuuza bidhaa zao na mazao hotelini.

Alibainisha kuwa mkakati wa kujenga hoteli kutaimarisha na kuongeza utalii wa mashamba ya zabibu unaohimizwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt Binilith Mahenge.

Amesema ujenzi wa hoteli utaongeza kasi ya utalii na matumizi ya kumbi za mikutano ambazo badala ya watu na taasisi mbalimbali kufanya mikutano jijini Arusha watakuja kufanya jijini Dodoma.

Mavunde alisema ujenzi wa hoteli utachangia maendeleo na siku si nyingi mikutano ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) itakuwa ikifanyika Dodoma badala ya Arusha.

Mhe. Mavunde aliipongeza serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli akisema maendeleo ya Dodoma yanatokana na juhudi na mkakati wa kuhamishia makao makuu ya nchi Dodoma ambako kumechangia kuongeza mahitaji mbalimbali yakiwemo ya huduma za kijamii.

Alisisitia kuwa kwa kitendho cha serikali kuhamia Dodoma, Baraza la Madiwani wa Jiji limechangamkia fursa hiyo kwa kuazimia kuwekeza katika kujenga hoteli na kitega uchumi katika mji wa serikali.

Meya wa Jiji la Dodoma, Profesa Davis Mwamfupe alisema utiaji saini wa mikataba hiyo miwili unatokana na kujitoa kwa watendaji wa jiji la Dodoma katika kutumia fedha za ndani kwa ufanisi.

Alikazia kuwa, pamoja na huduma hizo za jiji, pia wanatakiwa kupata mikopo kutoka benki mbalimbali mkoani na nchini kutekeleza mikakati hiyo ya kujenga mji wa serikali.

Alisema kwa mikopo hiyo, halmashauri ya jiji la Dodoma itafanikisha azma ya kujenga pia makao makuu ya serikali na kuifanya Dodoma kuwa jiji bora zaidi kwa ubora wa miundombinu.

Chanzo: 


Matangazo

  • TANGAZO LA MABADILIKO YA TAREHE YA USAHILI October 03, 2025
  • TANGAZO LA MAJINA YA WASIMAMIZI JIMBO LA MTUMBA October 03, 2025
  • MAJINA YA WASIMAMIZI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA- DODOMA MJINI October 03, 2025
  • TANGAZO LA MAJINA YA MAKARANI WAOGOZAJI WAPIGA KURA October 03, 2025
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Rc Senyamule awasihi wawekezaji sekta binafsi kuwekeza Dodoma

    October 03, 2025
  • CCTV kamera mwarobaini wa wavunjifu wa sheria jiji la Dodoma

    October 02, 2025
  • Wadau wa afya wapongezwa kwa juhudi zakudhibiti vifo vya wajawazito

    October 01, 2025
  • UONGOZI WA KLABU YA MICHEZO OFISI YA MKUU WA MKOA WA DODOMA WAKUTANA NA RAS KAZUNGU

    September 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.