• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji Dodoma kutoa Milioni 545 kwa vikundi - Mkurugenzi Mafuru

Imewekwa tarehe: October 21st, 2020

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeshatoa zaidi ya shilingi Bilioni tano kutoka asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kukopesha vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu katika jitihada za kuwawezesha kiuchumi.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru alipokuwa akifungua mafunzo kwa wajasiriamali watakaokopeshwa mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri katika ukumbi wa Shule ya sekondari Umonga.

Mafuru alisema “Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeshatoa shilingi Bilioni tano. Bilioni tano hizi mchango wake ni mkubwa kuliko inavyoweza kutegemewa. Katika msimu huu, tunaingiza kiasi cha Shilingi Milioni 545, ambazo zikiingia katika soko, ndani ya kipindi cha miezi mitatu hadi minne inaweza kuwa imeongeza sana maendeleo, hata kama hairudi kwa Jiji moja kwa moja ila mchango wake unasambaa sana kwa jamii na kuchochea ukuaji uchumi".

Mkurugenzi huyo, aliwataka wanavikundi kuwa na nidhamu katika matumizi ya fedha. “Nisisitize, kwenye vikundi hivi, tunamalezi tofauti na tabia tofauti. Ninachotaka kwenu ni nidhamu ya matumizi na utunzaji wa fedha. Mkifanikiwa ninyi Halmashauri yetu inakuwa imefanikiwa na malengo ya Serikali kufikiwa. Naamini hizi Bajaji na Pikipiki mtaendesha wenyewe, tunachotaka baada ya miezi sita, kama kikundi muweze kuajiri watu wengine ili wengi waweze kunufaika na hiyo shilingi Milioni 545.

Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeandaa mafunzo kwa vikundi 14 vya wajasiliamali wenye ulemavu, bodaboda na bajaji kabla ya kuvikopesha shilingi Milioni 545.

Awali mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Sharifa Nabalang’anya alipokuwa akimkaribisha Mkurugenzi wa Jiji kufungua mafunzo hayo alisema kuwa mafunzo hayo yametolewa kwa vikundi vya wajasiriamali ili kuwajengea uwezo wa kuendesha na kusimamia miradi.

“Ndugu Mkurugenzi mafunzo ambayo yanatolewa hapa yanawahusisha wakuu wa idara na wadau toka nje ya Halmashauri. Mweka Hazina wa Jiji ataeleza juu ya usimamizi fedha na uendeshaji wa miradi. Mkaguzi wa Ndani ataeleza juu ya wajibu wa vikundi tunavyovikopesha mikopo kutosababisha kuzalishwa kwa hoja za ukaguzi, ili tusipate hoja mpya” alisema Nabalang’anya.

Eneo lingine ni elimu ya ujasiriamali na utunzaji wa kumbukumbu ambalo wataalam wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wamejipanga vizuri kufundisha. “Mwanasheria atawaambia kuwa mikopo hii ipo kisheria. Kwa hiyo hata usimamizi wake upo kisheria na siyo mikopo ya kisiasa” alisisitiza Nabalang’anya.

Aidha, alisema kuwa lengo la Mheshimiwa Rais ni kutatua changamoto ya mitaji kwa makundi maalum. Wakati huohuo, kuhakikisha wananchi wa chini wanaimarika kiuchumi. Ndiyo maana baada ya Serikali ya awamu ya tano kuingia madarakani ikaondoa riba. Mikopo hii ilikuwa inahudumia makundi mawili tu, wanawake na vijana ila baada ya Serikali hii kuingia madarakani ikaongeza kundi la watu wenye ulemavu.

Kwa upande wake mnufaika wa mikopo hiyo, Lucy Ndahani aliishukuru Serikali kwa kutoa mikopo hiyo. “Napenda kutoa heshima kwa Mkurugenzi wa Jiji kututembelea, tunamshukuru sana kutujali sisi wanawake wenye ulemavu na kuwajali vijana na wanawake. Tunatoa shukrani kwa Rais Magufuli kututengea fedha kwa ajili ya kujiendeleza. Namshukuru sana Mungu kutupa viongozi hawa wema, namuomba Mungu awabariki sana” alisema Ndahani kwa hisia kali.

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Sharifa Nabalang’anya alipokuwa akiongea kumkaribisha Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kufungua mafunzo.


Wanufaika wa mikopo ya Halmashauri ya asilimia 10 wakimsikiliza Mkurugenzi wa Jiji (hayupo pichani) alipokuwa akifungua mafunzo kwa wajasiriamali.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.