• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji Dodoma laanza kutikisa kwa miradi

Imewekwa tarehe: August 27th, 2019

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imesaini mikataba ya ujenzi wa miradi ya kimkakati yenye thamani ya shilingi bilioni 69.29 katika jitihada zake za kuelekea kujitegemea kimapato.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi alipokuwa akitoa maelezo mafupi ya miradi ya kimkakati ya ujenzi wa hoteli ya Jiji la Dodoma na jengo la kitegauchumi la Jiji katika halfa ya utiaji saini mikataba miwili ya miradi ya uwekezaji Nyerere square leo.

Kunambi alisema kuwa Halmashauri ya Jiji inasaini mkataba wa ujenzi wa Hoteli ya Jiji la Dodoma (Dodoma City Hotel) itakayojengwa katika mtaa wa Nyerere na Mkandarasi Stecol Coorporation (China) kwa gharama ya shilingi bilioni 9.995. Alisema kuwa hoteli hiyo itakayokuwa na hadhi kati ya nyota tatu na nyota nne, itakuwa na ghorofa 11 ikiwa na kumbi za mikutano, mgahawa mkubwa, vyumba vya kulala na maegesho ya magari.

Mkataba wa pili aliutaja kuwa ni ujenzi wa jengo la kitegauchumi la Jiji (Government City Complex) litakalojengwa katika Mji wa Serikali – Mtumba. Jengo hilo litajengwa na Mkandarasi Mohamed Builders Ltd kwa gharama ya shilingi bilioni 59.3. “Jukumu la Halmashauri ya Jiji ni kujenga makao makuu ya nchi. Hivyo, awamu ya kwanza litajengwa jengo la ghorofa sita litakalokuwa na mgahawa, sehemu za taasisi za kifedha, na kumbi za mikutano zenye ukubwa tofauti na ‘apartments kwa gharama ya shilingi bilioni 18’” alisema Kunambi.

Miradi yote itajengwa kwa fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri. “Halmashauri ya Jiji tunataka ku-cross border kwenda mikoa mingine kuwekeza na hadi nje ya nchi. Fedha zipo ni fikra sahihi na uzalendo tu. Ndani ya mwaka mmoja watakabidhi miradi yetu” alisema Kunambi.

Katika salamu za Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo aliipongeza Halmashauri ya Jiji kwa ukusanyaji mapato ya ndani. “Hakuna Halmashauri yeyote nchini iliyoweza kukusanya shilingi bilioni 71. Halmashauri nyingine zinakusanya shilingi bilioni mbili na nyingine shilingi bilioni 30 kwa mwaka. Ninyi mnaweza kuwalipa mishahara na kuwatekelezea miradi ya maendeleo Halmashauri zingine mbili” alisema Jafo.

Nae mkuu wa mkoa wa Dodoma, Dkt Binilith Mahenge alisema kuwa Dodoma, inakabiliwa na changamoto ya uwekezaji katika shule za kimataifa, na kualika wawekezaji katika eneo hilo. Akiongelea ujenzi wa miradi ya kimkakati ya Halmashauri ya jiji, aliitaja kuwa ni sawa na ujenzi wa viwanda. “Hoteli hiyo ni sawa na kiwanda, utapata matumizi ya bidhaa zinazotoka Dodoma. Ukitumia mvinyo unamhamasisha mkulima wa zabibu kulima zaidi” alisema Dkt Mahenge.

Waziri wa TAMISEMI Mhe. Seleman Jafo akitoa nasaha kwa wakandarasi baada ya tukio la kusaini mikataba ya Ujenzi wa Majengo ya Vitegauchumi vya Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini leo.

Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma Profesa Davis Mwamfupe (wa pili kulia waliokaa) na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi (wa kwanza kulia waliokaa) wakiweka saini kwenye mtakaba wa Ujenzi wa 'Government City Complex' pamoja na wawakilishi wa Kampuni ya Mohamed Builders Ltd.

Mgeni rasmi wa tukio la utiaji saini wa Mikataba ya Ujenzi wa Majengo ya Vitegauchumi vya Jiji la Dodoma Mhe. Selemani Jafo (wa nne kutoka kushota waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge (wa tatu kushoto waliokaa), Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma (wa tatu kulia waliokaa), Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi (wa kwanza kulia waliokaa), Mbunge wa Jimbo la Dodoma (wa pili kulia waliokaa), wawakilishi wa Wakandarasi wa miradi ya vitegauchumi na viongozi mbalimbali waliohudhuria halfa ya utiaji saini miradi ya Jiji. 

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.