• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji Dodoma laongoza tena ukusanyaji mapato ghafi Tanzania

Imewekwa tarehe: August 15th, 2019

Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa mara nyingine tena imeongoza kwa ukusanyaji wa Mapato ya ndani kwa kukusanya mapato ghafi zaidi ya Halmashauri zote nchini.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mitaa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo alipokuwa akitoa tathmini ya ukusanyaji mapato kwa Halmashauri zote nchini kwa mwaka wa fedha 2018/19.

Aidha, kwa mara ya kwanza Nchini Halmashauri zote 185 zimefanikiwa kukusanya sh. bilioni 661.4 ambayo ni sawa na asilimia 91 ya malengo ya mwaka wa Fedha 2018/19 ya kukusanya sh bilioni 723.
Matokeo haya ni ongezeko la asilimia 9 kwa Mwaka wa Fedha 2018/19 ukilinganisha na makusanyo ya asilimia 81 ya Mwaka wa Fedha 2017/18 huku Halmashauri ya Jiji la Dodoma sambamba na Mkoa wa Dar es salaam zikiongoza kwa mapato ghafi.

Hayo yabamebainishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa alipokuwa akitoa  taarifa ya mapato na matumizi ya fedha za vyanzo vya ndani vya halmashauri kwa mwaka wa fedha 2018/19. Mapato haya ya ndani hayajumuishi vyanzo vinavyokusanywa na Serikali kuu.

Akifafanua zaidi Mhe. Jafo alisema halmashauri za Wilaya tano zilizoongoza kwa kigezo cha asilimia ya mapato ya ndani kuwa ni Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi (asilimia 171), Wanging’ombe (asilimia 165), Kilolo (asilimia 150), Misenyi (asilimia 142) huku Mbeya DC ikishika nafasi ya tano kwa kukusanya asilimia 141.

Halmashauri  za Wilaya zilizofanya vibaya kiasilimia ni Tandahimba DC (asilimia 19), Msalala (asilimia 19), Masasi DC (asilimia 26) Newala (asilimia 27) pamoja na Nanyumbu (asilimia 36).
Kwa kigezo cha pato ghafi, Mhe. Jafo alisema "halmashauri zilizoongoza kwa wingi wa mapato kuwa ni Halmashauri ya Jiji la Dodoma (Sh bilioni  71.7), Ilala (Sh bilioni 58.1), Kinondoni (Sh bilioni 34) Temeke  Sh bilioni 33.3), Ubungo (bilioni 18.6) na Jiji la Arusha (Sh bilioni 16.4) wakati halmashauri tano zilizofanya vibaya katika kundi hili ni Nanyamba (sh milioni 258), Gairo DC(Sh milioni 396), Kigoma DC (Sh milioni 397.1) Buhigwe (Sh milioni 403.8) na Kakonko DC (Sh milioni 403.8)".

Vilevile, katika kundi la mikoa kwa kigezo cha asilimia, Jafo alisema mikoa inayoongoza kwa kigezo cha asilimia ya mapato ya ndani ni Mkoa wa Geita (asilimia 119), Iringa (asilimia  117), Songwe (asilimia 112), Kagera (asilimia 105) na Njombe  (asilimia  104), wakati mikoa iliyofanya vibaya katika kundi hili ni Mtwara (asilimia 42), Simiyu (asilimia  45.9), Shinyinga (asilimia 62), Kigoma (asilimia 74) Mara na Morogoro (asilimia 80).

Kwa upande wa mikoa kwa kigezo cha pato ghafi, Mhe. Jafo alitaja Mikoa inayoongoza kuwa ni Dar es Salaam (Sh bilioni1 163.5), Dodoma (Sh bilioni 82.6), Mwanza (Sh bilioni 32.6) Arusha (Sh bilioni 31.9) na Mbeya (Sh bilioni 31.4) wakati mikoa iliyofanya vibaya katika kundi hili ni Katavi (Sh bilioni 7.3), Kigoma (Sh bilioni 7.7), Rukwa (Sh bilioni 8.2) Simiyu (Sh bilioni 8.8) na Njombe (Sh bilioni 11.4).
Tena, Jafo alisema Jiji la Arusha  limeongoza  katika kundi la halmashauri za majiji kwa asilimia kwa kukusanya asilimia 105 ya makisio huku jiji la Mbeya  likiwa la mwisho katika kundi hilo baada ya kukusanya asilimia 89 ya makisio.

Alisema Halmashauri ya Jiji la Dodoma inaongoza kwa kigezo cha pato ghafi ambapo imekusanya Sh bilioni 71.7 na halmashauri ya jiji la Mbeya imekuwa ya mwisho baada ya kukusanya Sh bilioni 11.4.
Zaid ya hayo, Jafo alisema halmashauri ya manispaa ya Sumbawanga imeongoza kundi la halmashauri za Manispaa kwa kukusanya asilimia 138 ya makisio huku Lindi ikishika nafasi ya mwisho kwa kukusanya asilimia 54 ya makisio.

Jafo alisema kwa upande wa halmashauri ya Manispaa ya Ilala imeoongoza katika kundi la halmashauri za Manispaa kwa kigezo cha mapato ghafi baada ya kukusanyw Sh bilioni 58 huku Lindi ikiwa ya mwisho kwa kukusanya Sh bilioni 1.0.

Aidha, Jafo alisema halmashauri ya Mji wa Geita imeongoza kundi la halmashauri za miji kwa kigezo cha asilimia ambapo wamekusanya kwa asilimia 157 ya makisio huku halmashauri ya Mji wa Nanyamba imekuwa ya mwisho baada ya kukusanya asilimi 11 ya makisio.

“Katika kigezo ya pato ghafi kwa halmashauri za mji, Geita inaongeza baada ya kukusanya Sh bilioni 8.02 na halmashauri ya mji wa Nanyamba imekuwa ya mwisho ikiwa imekusanya Shilingi milioni 257.6.
Kwa upande wa halmashauri za wilaya, Jafo alisema Mbozi inaongoza kwa kukusanya kwa asilimia 171 ya makisio na ya mwisho ni Tandahimba iliyokusanya asilimia 19 ya makisio wakati kwa upande wa pato ghafi, Chalinze inaoongoza kwa kukusanya Sh bilioni 7.6 na ya mwisho katika kundi hili ni Gairo  iliyokusanya Sh milioni 396.1.

Vilevile, Jafo aliwataka wakurugenzi ambao Halmashauri zao zimefanya vibaya katika ukusanyaji wa mapato kujitathimini na kuweka mikakati ya kuongeza vyanzo vya mapato na mapato ya halmashauri zao kwa ujumla.

Pia Waziri Jafo aliwaagiza Wakurugenzi ambao Halmashauri zao zimetoa mikopo ya wanawake, vijana na walemavu chini ya asilimia 50 kuandika barua za maelezo kwanini wasichukuliwe hatua kwa kuvunja sheria na barua hizo ziwasilishwe ndani ya muda wa wiki mbili.

Aliongeza kuwa Wakurugenzi wote wahakikishe  ukusanyaji wa mapato hayo ya ndani unaenda sambamba na upelekaji wa fedha kwenye miradi ya maendeleo na mikopo kwa wanawake, vijana na walemavu.
Hata hivyo, Mhe. Jafo ameendelea kusisitiza matumizi ya mifumo ya kielektroniki katika ukusanyaji wa mapato ya ndani ili kuzuia upotevu wa mapato hayo.

Chanzo: tovuti ya tamisemi : (www.tamisemi.go.tz)



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.