• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji Dodoma laweka mkakati wa kupambana na maambukizi mapya ya Kifua Kikuu

Imewekwa tarehe: March 24th, 2020

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeamua kutoka ofisini na kuwafuata wagonjwa wa kifua kikuu na kuwaanzishia tiba katika mkakati wa kupambana na maambukizi mapya kwa jamii.

Mkakati huo ulitajwa na mratibu wa kifua kikuu na ukoma wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Peres Lukango (pichani) alipokuwa akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake leo jijini Dodoma.

Dkt. Lukango alisema kuwa Halmashauri ya Jiji imeweka mikakati mbalimbali ya kukabiliana na ugonjwa wa kifua kikuu. “Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika kukabiliana na ugonjwa wa kifua kikuu, tumeamua kutoka ofisini na kuwafuata washukiwa wa ugonjwa wa kifua kikuu huko walipo. Tofauti ya zamani tulikuwa tunawasubiri wagonjwa waje katika vituo vya afya. Sasa hivi, tunawatafuta, kuwafikia, kuwachunguza na wanapobainika tunawaanzishia huduma ya matibabu hadi wapone” alisema Dkt. Lukango. Njia hiyo inasaidia kuwafikia wagonjwa wengi kwa sababu wengine hukosa nauli ya kwenda katika vituo vya afya kwa ajili ya uchunguzi, aliongeza.

Halmashauri imekuwa ikitumia wahudumu wa afya ngazi ya jamii kwenye mapambano dhidi ya kifua kikuu. Wahudumu hao wamekuwa wakiwasaidia wagonjwa wa kifua kikuu katika huduma za tiba.

Mratibu huyo alisema kuwa elimu imeendelea kutolewa katika Halmashauri ya Jiji ili kuhakikisha wananchi wote wanafikiwa na elimu ya kujikinga na ugonjwa wa kifua kikuu. “Madaktari wa pembezoni tumewajengea uwezo wa kubaini wagonjwa wa kifua kikuu wanapofika katika vituo vyao. Njia bora ya kubaki salama ni kutibu ugonjwa huo” alisema mratibu huyo. Vilevile, aliitaka jamii kuhakikisha nyumba na maeneo ya kazi yanakuwa na hewa ya kutosha inayozunguka na mwanga kwa sababu mwanga unasaidia kuua vimelea vya kifua kikuu.

Elimu inayoendelea kutolewa inajikita katika kuyalinda makundi ambayo yapo katika hatari ya kupata ugonjwa huo. Aliyataja makundi hayo kuwa ni wazee kutokana na kinga zao kuwa zinashuka. Kundi lingine ni watoto wadogo kutokana na kinga zao kuwa hazijakomaa. Makundi mengine ni watu wanaougua magonjwa sugu kama kisukari, saratani na utapiamlo.

Aidha, aliwashukuru wafadhili wanaofadhili upatikanaji wa dawa hizo. “Shukrani kwa wafadhili wa kifua kikuu, kwa sababu wanawezesha dawa hizo kutolewa bure kwa wagonjwa. Unajua matibabu ya kifua kikuu ni miezi sita, hivyo ni gharama kubwa kama mgonjwa angekuwa ananunua dawa hizo mwenyewe. Ugonjwa huu bahati mbaya zaidi unawaathiri zaidi watu wa kipato cha chini na uwezo wa kufanya kazi unapungua sana” alisema Dkt. Lukango.

Akiongelea hali ya kifua kikuu katika Jiji la Dodoma, Dkt. Lukango alisema kuwa mwaka 2019 halmashauri iliwekewa lengo la kuibua wagonjwa zaidi ya 1500 na wagonjwa walioibuliwa ni zaidi ya 1450 lengo hilo lilifikiwa kwa asilimia 90. “Mwaka 2020 tumepewa lengo la kuibua wagonjwa zaidi ya 2000 likiwa ni lengo kubwa kuliko Halmashauri zote za Mkoa wa Dodoma. Hadi sasa tumeibua wagonjwa zaidi ya 430 na juhudi zinaendelea vizuri” alisema Dkt. Lukango.

Nae Dkt. Raymond Ndolele alisema kuwa wagonjwa wanaopatikana na kuanza matibabu hufuatiliwa hadi wamalize matibabu. “Wagonjwa tunaowapata huwa tunafanya ufuatiliaji kwenye familia zao ili kubaini kama wameambukiza watu wengine ili wote waanze matibabu ya kuwakinga.

Kwa upande wake muuguzi Foibe Nonya alisema kuwa wagonjwa wa kifua kikuu wanaohudumiwa dozi ya kwanza ni miezi mwili, na kuendelea na miezi minne inayobaki.

Muhudumu wa afya ngazi ya jamii, Rose Lema alisema kuwa wamekuwa wakitoa elimu ya lishe kwa wagonjwa wa kifua kikuu ili kuwasaidia kuwa na afya njema katika kipindi chote wanachoendelea na matibabu.

Maadhimisho ya siku ya mapambano ya kifua kikuu mwaka 2020 yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Wakati ni huu, tuunganishe nguvu na kuwajibika katika mapambano ya kutokomeza kifua kikuu”

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.