• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji, FAO wamwaga neema wakulima Kikombo

Imewekwa tarehe: June 16th, 2021

Na Nemes Michael, DODOMA

SHIRIKA la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) kwa kushirikiana na Halmashari ya Jiji la Dodoma wameahidi kutatua changamoto za miundombinu ya maji katika mradi wa umwagiliaji, na upatiknaji wa elimu stahiki ya kupambana na wadudu katika kata ya Kikombo.

Kauli hiyo imetolewa na Mwakilishi Msaidizi Mkazi wa shirika hilo nchini Tanzania Charles Tulai wakati wa makabidhiano ya mbegu bora kwa wakulima wa kikundi cha Ilolo kilichopo mtaa wa Kikombo Makulu pamoja na pikipiki kwa Afisa Kilimo wa kata ya Kikombo.

Akizungumza katika mkutano huo, Tulai alisema kuwa ushirikiano walionao na Halmashairi ya Jiji la Dodoma ni mkubwa na wenye lengo la kuhakikisha utekelezaji chanya wa shughuli katika sekta ya kilimo.

“Ulaji katika dunia nzima hasusan ya ulimwengu wra tatu huku Afrika, bado hatujafikia hatua ya lishe inayotakiwa, tunasahau vitu muhimu kama matunda na mboga, hichi kikundi kimenifanya nije kwa sababu kimenipa hamasa na naamini wengi watajifunza kupitia kwenu, hakika mnastahili pongezi” alisema Tulai.

Tulai aliongeza kuwa, mbegu zilizoletwa ni mbegu sahihi katika kuhakikisha tunaboresha afya zetu binafsi na vipato vyetu, na kwa hatua hii naamini wakulima wa Kikombo Makulu watakuwa mfano kwa wakulima wengine katika kilimo kisichotegemea mvua na chenye mavuno ya kutosha.

Kwa upande wake, Afisa Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika wa Jiji la Dodoma, Yustina Munishi ambaye alimwakilisha Mkurugenzi wa Jiji hilo Joseph Mafuru, aliliishukuru FAO na kwamba  ushirikiano ulipo baina ya taasisi hizo umekuwa mzuri na wenye mafanikio.

“Ushirikiano huu ni wa muda na wenye mafanikio, hatua tulizofikia kwa kuleta mbegu sahihi na elimu katika kilimo cha umwagiliaji ni hatua nzuri katika kuhakikisha tunatetea afya za wananchi na kuongeza kipato binafsi cha mkulima na Taifa kwa ujumla” alisema Munishi.

Naye, Afisa Kilimo Kata ya Kikombo Madei Kidarya alilishukuru shirika la FAO na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kukabidhiwa pikipiki ambayo itamsaidia katika usafiri na urahisishaji wa huduma kwa wakulima wa kata hiyo.

Mmoja wa wanakikundi cha wakulima kilichonufaika na mbegu hizo Martha Ramadhani alisema kuwa, hapo awali hali haikuwa sawa kutokana na aina ya mbegu zilizokuwa zinatumika, ila sasa kupitia mbegu bora walizokabidhiwa anaamini kutakuwa na maendeleo chanya katika kuimarisha afya na kuinua uchumi kwa wakulima na Taifa.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.