• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji kuonesha teknolojia za kisasa za kilimo na mifugo Nanenane

Imewekwa tarehe: July 29th, 2020

WATANZANIA wameshauriwa kujitokeza kwa wingi kutembelea banda la Halmashauri ya Jiji la Dodoma kujifunza matumizi ya teknolojia ya kisasa katika shughuli za kilimo na mifugo kwa lengo la kukuza uchumi kupitia shughuli za kilimo na mifugo kibiashara na kuboresha usalama wa chakula.

Wito huo umetolewa na mkuu wa idara ya kilimo, umwagiliaji na ushirika wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Yustina Munishi (pichani juu) alipokuwa akiongelea maandalizi ya maonesho ya shughuli za kilimo na mifugo ya Nanenane yatakayofanyika katika viwanja vya Nanenane eneo la Nzuguni jijini Dodoma.

Munishi amesema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma imedhamiria kuwaonesha watanzania matumizi ya teknolojia mbalimbali za kuwasaidia kukuza uchumi kupitia shughuli za kilimo na kukifanya kilimo kuwa cha kibiashara na kuboresha usalama wa chakula. “Halmashauri ya Jiji la Dodoma tumejipanga kuleta mabadiliko kupitia kilimo na kukifanya kilimo kiwe kibiashara, katika eneo letu la banda la Nanenane tumeweka mfumo wa umwagiliaji maji kwa njia ya matone ili watanzania waweze kujionea matumizi ya maji kidogo katika shughuli za kilimo.

Amesema kuwa katika kuonesha teknolojia hizo, zitahusisha matumizi yake katika mazao ya bustani. “Unajua mazao ya bustani ni mazao yenye thamani kubwa sana. Mfano, vitunguu, tutaonesha teknolojia ya kuzalisha vitunguu kwa njia bora na kupata tija. Ukizalisha vitunguu kwenye ekali moja unaweza pata mavuno tani 19 hata na zaidi” alisema Munishi.

Mkuu huyo wa Idara ya kilimo, umwagiliaji na ushirika alisema kuwa Halmashauri inataka kuwainua wananchi kupitia kilimo cha mbogamboga kibiashara. “Katika banda la Jiji la Dodoma, wananchi watafundishwa kulima kibiashara chainizi, kabichi, spanishi, bilinganya, sukumawiki, karoti na mazao mengine mengi. Mazao haya yanaonesha jinsi mwananchi anavyoweza kukuza kipato chake. Tayari wananchi wa maeneo ya Ihumwa, Kikombo na Matumbulu wanazalisha mbogamboga kwa kiwango kikubwa na kuuza nje ya Wilaya ya Dodoma. Haya ni mafanikio makubwa katika dhana ya kukuza uchumi kupitia kilimo” alisema Munishi kwa furaha.

Ikumbukwe kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilishika nafasi ya kwanza kwa Halmashauri zote nane za Mkoa wa Dodoma katika maonesho ya Nanenane mwaka 2019.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.