• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji la Dodoma kuendeleza ushirikiano na taasisi ya IITA

Imewekwa tarehe: April 23rd, 2021

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeahidi kuendelea kushirikiana na Taasisi ya Kilimo ya Kimataifa ya Mabadiliko ya Tabia ya Nchi (IITA) kama mkakati wa kutoa elimu ya kilimo himilivu kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi ili kuwahikikishia wananchi uhakika wa chakula.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Yustina Munishi wakati akihitimisha ziara ya siku ya wakulima katika kata ya Hombolo Bwawani jijini hapa.

“Halmashauri ya Jiji la Dodoma itaendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali ikiwemo taasisi ya kilimo ya kimataifa ya mabadiliko ya tabia ya nchi (IITA) katika kutoa elimu juu ya kilimo himilivu kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi.” Alisema kuwa kilimo hicho kinawasaidia wakulima kupata mazao mengi wakati mkulima hatumii nguvu nyingi katika uzalishaji wa mazao.

Munishi alisema kuwa wakulima wanapaswa kuzingatia mafunzo kwa malengo ya sasa na ya baadae kwa sababu kilimo ni uti wa mgongo. Alisema kuwa kupitia mafunzo hayo, mkulima anaweza kujikwamua kimaisha kwa kufanya kilimo cha kibiashara kupitia mbinu mbadala za kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi.

Akiongelea muendelezo wa mashamba darasa katika Jiji la Dodoma, alisema “Halmashauri ya Jiji la Dodoma imejipanga kuhakikisha kwamba mashamba darasa yanakuwepo maeneno yote ya kata ambazo ni za kilimo. Tunazo kata 24 za kilimo na tumeweza kuchukuwa kwanza maafisa kilimo wetu wote kuwaleta kwenye ziara ya mafunzo katika shamba darasa lililopo Hombolo Bwawani, lakini katika msimu wa kilimo wa mwaka 2021 / 2022 tumetenga bajeti kwa ajili ya ununuzi wa mbegu” alisema Munishi.

Kwa upande wake, Afisa Kilimo wa kata ya Hombolo Bwawani, Paschal Sabunyoni alisema kuwa mafunzo kupitia shamba darasa hayakuwepo awali. Kupitia Halmashauri ya Jiji la Dodoma uanzishaji wa mashamba darasa umesaidia katika kuhimili mabadiliko ya tabia ya nchi kwa kufanya kilimo himilivu.

“Mwanzo wakulima walikuwa wanaeleza kuwa walikuwa hawazifahamu njia vizuri. Lakini kupitia shamba darasa wamejifunza mengi katika uandaaji wa mashamba, utumiaji wa mbolea na maandalizi ya vifaa katika kilimo kulingana na aina ya mazao, pia utumiaji wa mbegu zilizo bora” alisema Sabunyoni.

Ziara ya siku ya wakulima kata ya Hombolo Bwawani jijini Dodoma ilifanyika katika Mtaa wa Hombolo Bwawani B, ikiongozwa na Mkuu wa idara kilimo, umwagiliaji na ushirika wa Jiji la Dodoma, wataalamu kutoka taasisi ya IITA, Diwani wa Kata ya Hombolo Bwawani, na viongozi waandamizi wa Kata hiyo na wakulima.

Mkuu wa idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Yustina Munishi akiongea na mwandishi wetu mara baada ya ziara ya kutembelea shamba darasa.

Shamba darasa lililotembelewa na wataalam wa kilimo lililoko Mtaa wa Hombolo Bwawani B Jijini Dodoma.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.