• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji la Dodoma kuingia ubia utekelezaji Miradi

Imewekwa tarehe: February 3rd, 2025

Na. Halima Majidi, DODOMA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma katika kuhakikisha inaimarisha na kukuza wigo wa ukusanyaji wa mapato kwa maendeleo yake na nchi kwa ujumla imeainisha miradi ya kuingia ubia na kushirikisha sekta binafsi na za umma.

Akizungumza katika Mkutano wa Baraza la Madiwani wa kupitia mapendekezo ya rasimu ya Mpango na Bajeti ya Mwaka 2025/2026, uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani, Prof. Davis Mwamfupe, alisema kuwa halmashauri imekuja na mkakati mpya wa kujiweka tayari kwa kufanya miradi kwa ubia kupitia mfumo wa ushirikishaji sekta binafsi na sekta ya umma (PPP).

Prof. Mwamfupe alisema kuwa miradi mingi imewekwa katika masoko ili kuweza kuita na kuvutia sekta binafsi ili waweze kushiriki na kuwekeza katika miradi hiyo. “Kwa kuangalia miradi ambayo tulikuwa nayo kipindi cha nyuma na kwa kujifunza kutokana na hiyo tumepata tabu sana kukamilisha miradi miwili ya hoteli. Kwahiyo, tumeweka mkakati mpya wa kushirikisha sekta binafsi na za umma ili kurahisisha ufanisi wa miradi hiyo”, alisema Prof. Mwamfupe.

Aidha, Prof. Mwamfupe alisema kuwa wamefanikiwa kuanzisha kampuni Special Purpose Vehicle (SPV) ambayo ni chombo cha kuendesha miradi ambayo inahusiana na biashara kwa lengo la kutanua wigo wa mapato. Aliongeza kuwa “majukumu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma si sana kufanya biashara. Lakini tunajikuta tunamiradi inayofanya biashara ili kuondoa ukinzani wa namna hiyo tukasisitiza kuwa na mfumo huo pale tunapokuwa na miradi ambayo inaingiza fedha. Pale tunapokuwa na miradi ambayo ubunifu wake unahitaji utaalamu uliopo nje ya uwezo wetu ndio maana tukaona SPV haikwepeki” alisema Prof. Mwamfupe.

Sambamba na hilo, alisema kuwa serikali imeweka adhma ya kuanzisha mji katika eneo la Hombolo Bwawani ikiwa ni katika muendelezo wa mipango miji wa 2019-2039. “Eneo lile lina mandhari nzuri. Hivyo, kutenga maeneo na kujenga mji wa kisasa wenye miundombinu bora na huduma muhimu kwa lengo la kuvutia wageni pamoja na kukuza sekta ya utalii. Tunadhani masaki ya Dodoma itakuwa uekekeo wa namna hiyo”, alisema Prof. Mwamfupe.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Makole, Omari Haji Omari, alisema anaupongeza uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kuweka mkakati wa ujenzi wa mji mpya wa kipekee Hombolo Bwawani kwasababu sehemu hiyo itawasaidia watu kupata mahitaji yao ya muhimu. “Mtu hatakuwa na sababu ya kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam kwaajili ya kufurahi yaani 'kuenjoy' badala yake ataenda Hombolo Bwawani” alisema Omari.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.