• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

"Jiji la Dodoma kuongoza usafi" - Kunambi

Imewekwa tarehe: May 31st, 2019

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imejipanga kuongoza katika usafi wa mazingira kwa upande wa Halmashauri za Majiji kutokana na nafasi yake ya kimkakati nchini.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi alipokuwa akielezea mipango ya Jiji hilo kuhusu usafi wa mazingira muda mfupi kabla ya Mkuu wa Wilaya ya Dodoma kuzindua kituo cha kupokelea mifuko ya plastiki kilichopo katika kata ya Uhuru.

Kunambi alisema kuwa, Halmashauri ya jiji la Dodoma imejipanga kuongoza katika upande wa Majiji nchini kwani Dodoma ni Makao Makuu ya nchi, hivyo suala la usafi ni agenda ya kudumu. 

“Halmashauri ya Jiji la Dodoma tumejipanga vizuri ambapo tumekuwa tukitoa elimu ya usafi wa mazingira na madhara ya mifuko ya plastiki kuanzia ngazi ya mitaa, kata hadi wilaya” alisema Kunambi.

“Mheshimiwa mkuu wa Wilaya, Halmashauri ya Jiji la Dodoma tunaenda kuongoza na kuwa wa mfano Tanzania, tumekuwa na utamaduni wa kuongoza katika mapato, usafi, afya, elimu, sababu kubwa sisi wote ni vijana...tunafikiria miaka 50 ijayo ya siyo miaka 50 iliyopita” alisema Kunambi.

 Aidha, aliwapongeza wakazi wa Jiji la Dodoma kwa utulivu na ushirikiano wanaoendelea kumpatia katika kutekeleza majukumu yake.

Akiongelea juu ya utii wa sheria, aliwataka wananchi wa Jiji hilo kutii sheria bila shuruti na kusema kuwa usafi wa mazingira ni jukumu la kila mtu. 

“Katika nyumba yako au eneo unalofanyia shughuli zako, hakikisha hakuna mfuko wa plastiki unaozagaa” alisema Kunambi.  

Kuhusu taasisi zinazokaidi kutoa tozo kwa ajili ya ubebaji taka na usafi wa mazingira, mkurugenzi huyo alionesha masikitiko yake kwa baadhi ya taasisi hizo na kusema zinakwamisha juhudi za usafi wa mazingira. “Wengine wanafikiria usafi siyo sehemu yao. Zipo taasisi kubwa hazilipi tozo ya usafi wa mazingira. Tusimame pamoja ili kusafisha jiji letu” aliongeza Kunambi.

Aidha, Mkuu wa idara ya Mazingira na udhibiti taka ngumu katika jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alisema kuwa Halmashauri hiyo ilijikita katika kutoa elimu kuanzia ngazi ya Mtaa, Kata na Wilaya juu ya katazo la serikali la matumizi ya mifuko ya plastiki na kuelezea mifuko mbadala. Alisema kuwa elimu hiyo ilitolewa kupitia njia mbalimbali za mawasiliano kuanzia mitandao ya kijamii hadi vituo vya runinga.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.