• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

JIJI LA DODOMA LAJENGA SHULE YA SEKONDARI MIYUJI B ENEO LA KIMKAKATI

Imewekwa tarehe: December 3rd, 2023

Na. Josephina Kayugwa, MIYUJI

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imechagua kimkakati eneo la ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari Miyuji B ili kuweza kuwahudumia wananchi wengi.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alipokuwa akitoa maelezo ya utangulizi kwa Kamati ya Siasa Mkoa wa Dodoma iliyotembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari Miyuji B iliyopo Kata ya Miyuji jijini Dodoma.

Alhaj Shekimweri alisema kuwa eneo la ujenzi wa shule hiyo limechaguliwa kimkakati katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kuwa katikati ya maeneo ya wananchi na karibu na eneo zitakapojengwa nyumba 3,500 na Wakala wa Ujenzi Tanzania (TBA).

“Niwapongezi Diwani wa Kata ya Miyuji, Mheshimiwa Beatrice Ngerangera na Mkuu wa shule ya Miyuji, Mwl Greyson Maige kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa shule hii. Tulishauri pia kisima kuchimbwa katika eneo hili kwa lengo la kupata maji ya uhakika. Jukumu la wazazi sasa ni kuwapeleka shule watoto wao na kutafsi elimu watakayoipata kwenye fursa ya ajira” alisema Alhaj Shekimweri.

Akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari Miyuji B, Mkuu wa Shule ya Sekondari Miyuji, Greyson Maige alisema kuwa shule hiyo inakwenda kuwaondolea hadha wanafunzi ya kutembea umbali mrefu na kufika shuleni kwa wakati. Faida za mradi huu utakapokamilika ni kuwasaidia wanafunzi waliokuwa wakitembea umbali mrefu kutembea umbali mfupi na kufika shule kwa wakati. “Faida nyingine ni kupunguza idadi ya wanafunzi Shule ya Sekondari Miyuji ilipo Kata ya Mnadani na kupunguza mimba za utotoni pamoja na utoro wa wanafunzi. Kwa upande wa walimu watakaa kwenye mazingira ya shule na hivyo kuongeza ufanisi katika utendaji kazi na kuwezesha mazingira mazuri ya kuishi kwa walimu” alisema Mwl. Maige.

Shule ya Sekondari Miyuji ilipokea kiasi cha fedha shilingi 544,225,626 tarehe 30 Juni, 2023 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya katika Kata ya Miyuji iliyopo eneo la Mpamaa kupitia mradi wa SEQUIP (Mradi wa uboreshaji wa miundombinu ya elimu).

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.