• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji la Dodoma lakopesha vijana zaidi ya Bil. 1.1

Imewekwa tarehe: August 25th, 2021

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imekopesha shilingi 1,108,000,000 kwa vikundi 61 vya vijana katika utekelezaji wa mkakati wake wa uwezeshaji vijana kiuchumi kupitia asilimia nne za mikopo itokanayo na mapato ya ndani ya halmashauri kwa mwaka wa fedha 2020/2021.

Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Maendeleo ya Vijana wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mufungo Manyama alipokuwa akiwasilisha mada ya fursa za vijana katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika kikao cha wadau wa afua za afya ya uzazi na maendeleo ya vijana kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma leo.

Manyama alisema kuwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021, halmashauri ilitoa mikopo kwa vikundi 61 vya vijana yenye thamani ya shilingi 1,108,000,000. Alisema kuwa fedha hizo zilitolewa kugharamia miradi ya uwezeshaji vijana kiuchumi. “Miradi hiyo iligawanyika katika sekta za kilimo cha bustani za mbogamboga na matunda, ufugaji, ufundi, bodaboda, biashara ndogondogo. Sekta nyingine ni usindikaji wa vyakula, ujenzi, huduma za vyakula na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano” alisema Manyama.

Akiongelea utaratibu na sifa za kupata mikopo hiyo ya asilimia nne kwa vijana, alisema kuwa halmashauri inatoa mikopo hiyo yenye masharti nafuu kwa vijana waliojiunga katika vikundi vya watu watano na kuendelea. “Vikundi hivyo lazima viwe vimesajiliwa na vina vijana kuanzia umri wa miaka 15-35 na wawe na akaunti benki. Vikundi hivyo, lazima viwe na maandiko mafupi ya miradi yatakayoonesha mradi unaoombewa fedha na gharama zake” alisema Manyama kwa msisitizo.

Awali akitoa neno la utambulisho, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Asha Vuai alisema kuwa changamoto kuwa iliyopo ni kuwafanya vijana waweze kujitambua na kuwa wawajibikaji katika jamii. “Baadhi ya vijana siyo waaminifu hasa kwenye kufanya marejesho ya mikopo wanayokopa. Tofauti na akina mama, wengi ni waaminifu kwenye kufanya marejesho ya mikopo. Hata ukiangalia kwenye madeni, wengi wanaodaiwa ni vijana. Serikali ina lengo zuri la kuwawezesha vijana kiuchumi ndiyo sababu mikopo hiyo haina riba” alisema Vuai kwa masikitiko.

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Asha Vuai (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na baada ya kikao cha wadau wa afua za afya ya uzazi na maendeleo ya vijana kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.