• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji la Dodoma latekeleza agizo la Waziri Jafo Nanenane

Imewekwa tarehe: July 30th, 2020

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imetekeleza agizo la Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Selemani Jafo la kuzitaka Halmashauri zote nchini kuwa na vipando katika eneo la maonesho ya Nanenane kwa mwaka mzima ili wananchi wapate fursa ya kujifunza.

Kauli ya utekelezaji huo ilitolewa na Mkuu wa Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika, Yustina Munishi alipokuwa akiongelea utekelezaji wa agizo hilo ofisini kwake jana.

Munishi alisema “mtakumbuka wakati akifunga maonesho ya Nanenane mwaka 2019/2020 katika viwanja vya maonesho vya Nanenane, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Selemani Jafo aliziagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha zinakuwa na vipando mwaka mzima. Uwepo wa vipando hivyo utawawezesha wananchi kupata fursa pana zaidi ya kujifunza tofauti na kusubiri msimu wa maonesho ya Nanenane. Sisi tumetekeleza agizo hilo na kuweka katika mipango yetu. Utekelezaji wa agizo hilo pia ni utekelezaji wa Ilani ya chama kilichopo madarakani kwamba wananchi wawezeshwe kupata teknolojia bora za kilimo”.

Akiongelea uendelevu wa agizo hilo, alisema kuwa Halmashauri imechimba kisima kirefu katika eneo la maonesho ya Nanenane kwa lengo la kuwa na uhakika wa maji. Katika bajeti ya 2019/2020 shilingi milioni 40 ziliwezesha kuweka pampu na tenki la kuhifadhia maji na kuweka miundombinu ya umwagiliaji kwa njia ya matone, aliongeza.

Halmashauri imefanikiwa kuwajengea uwezo wananchi katika matumizi ya teknolojia katika kilimo cha nyanya. “Tunaweza kuzalisha nyanya kwa njia ya kitalu nyumba, na tumetoa elimu hiyo kwa wananchi juu ya matumizi ya kitalu nyumba. Katika awamu ya kwanza jumla ya vijana 100 wamepewa mafunzo ya matumizi ya teknolojia ya kitalu nyumba. Tunaona hiyo ni njia pekee ya kuwafundisha vijana matumizi ya teknolojia ili kuleta tija katika kilimo na kupata fursa za kiuchumi kwa sababu unalima eneo dogo lakini unazalisha kwa tija kubwa” alisema Munishi.

Aidha, alitoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kutembelea banda la Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika maonesho ya Nanenane ili kunufaika na elimu inayotolewa bure kuhusu kilimo, mifugo na uvuvi.

Maonesho ya Nanenane mwaka 2020 yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Kwa Maendeleo ya kilimo, Mifugo na Uvuvi, chagua viongozi bora 2020”.

Kwa upande wa kijana kutoka kikundi cha Maarifa John Samweli alisema kuwa mafunzo hayo yamewasaidia kupata uelewa wa matumizi ya teknolojia ya kitalu nyumba katika kilimo cha nyanya, pilipili hoho na matango. “Mafunzo haya yatatusaidia kujitegemea hata nje ya kikundi hiki, tunaishukuru Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kutupatia mafunzo ya mwezi mmoja na mkopo wa shilingi milioni saba (7,000,000).

Bustani ya Vitunguu maji.

Kitalu nyumba kwa kilimo cha ndani

Zao la mtama

Kabichi

Zao la Alizeti




Zao la bilinganya




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.