• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji la Dodoma limepunguza utegemezi wa kibajeti katika chanzo cha mauzo ya viwanja

Imewekwa tarehe: January 19th, 2024

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imepunguza utegemezi wa kibajeti katika chanzo cha mauzo ya viwanja kwa shilingi bilioni 11 ikijipanga kuboresha huduma kwa mwananchi analeyengwa moja kwa moja na bajeti hiyo.

Kauli hiyo ilitolewa na Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe katika Mkutano wa Baraza la Madiwani maalum kwa ajili ya kujadili rasimu ya Mpango na Bajeti wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa mwaka wa fedha 2024/2025 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Prof. Mwamfupe alisema “katika bajeti hii ni kupunguza utegemezi katika chanzo cha mauzo ya viwanja. Katika bajeti iliyopita tulikuwa na shilingi bilioni 29 tunazitegemea katika mauzo ya viwanja. Leo hii tumepunguza hadi shilingi bilioni 18. Napenda niwasisitizie wataalam wetu, mahitaji ya viwanja hayajapungua kwa kiasi kikubwa sana. Bado wananchi wanahitaji viwanja. Sekta ya ujenzi inazidi kushamiri kila asubuhi. Sehemu kubwa ambayo inadibi tuweke mkazo ni kuboresha huduma ili watu wavutike na viwanja tunavyouza sisi badala ya kwenda kwenye viwanja vingine ambavyo havina uhakika. Kama leo katika zoezi la kliniki tuliweza kutoa vibali vya ujenzi 4,470 kwa kipindi cha mwezi Oktoba hadi Desemba, 2023 tunataka tuwe na kasi hiyohiyo tuliyoanza nayo tuendelee nayo. Sisi ndiyo wenye ardhi, jukumu la kupanga na kumilikisha ardhi ni letu”.

Mstahiki Meya alisema kuwa bajeti hiyo imemlenga mwananchi wa kawaida moja kwa moja. “Ndiyo maana tukaweka mkazo mkubwa katika sekta ya elimu na afya. Katika bajeti hii tumejikita zaidi kukamilisha miradi viporo ambavyo ni kipaumbele ili kuunga juhudi za wananchi katika maeneo ya pembezoni mwa halmashauri yetu. Bajeti ni ukusanyaji wa mapato na matumizi. Tusipokusanya hatuna cha kutumia, lakini sisi tunaamini kwa nguvu tuliyoanza nayo tunaamini sana wote tutafanikiwa. Mkurugenzi tungependa kusikia upimaji kazi wa watendaji kwa maafisa wako unajikita wameshiriki namna gani katika ukusanyaji mapato” alisema Prof. Mwamfupe.

Mwenyekiti huyo alimshukuru Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kwa miongozo yake kwa halmashauri. Vilevile, alimshukuru Mkuu wa Wilaya ya Dodoma kwa jinsi anavyoishauri halmashauri na kusema uelewa wake kwa masuala ya halmashauri hauna kifani.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.