• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji la Dodoma linatambua jitihada zinazofanywa na mwanamke wa kijijini

Imewekwa tarehe: October 18th, 2023

Na. Dennis Gondwe, CHIHANGA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma inatambua jitihada zinazofanywa na mwanamke wa kijijini katika uzalishaji wa chakula na kusimamia lishe ya familia.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Charity Sichona alipokuwa akiongea maadhimisho ya siku ya mwanamke anayeishi kijijini ofisini kwake leo ambayo yatafanyika katika Kata ya Chihanga jijini Dodoma.

Sichona alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma inaadhimisha siku hiyo kwa lengo la kuendelea kutambua jitihada za mwanamke anayeishi kijijini. “Wanawake wanaoishi vijijini wanamchango mkubwa katika kuzalisha chakula na kuchangia uwepo wa chakula katika familia na nchi nzima. Hivyo, serikali imeamua kutambua jitihada zao za kilimo, ufugaji na shughuli za kiuchumi na kuwatia moyo ili waendelee kuzalisha wakati serikali ikiendelea kutatua changamoto zinawakabili” alisema Sichona.

Sichona alisema kuwa mwanamke wa kijijini anapowezeshwa kufanya shughuli zake bila vikwazo familia, halmashauri na taifa kwa ujumla litakuwa na uhakika wa chakula na hadi kuwa na chakula cha akiba. “Mwanamke ni mtendaji mzuri katika kazi za uzalishaji. Hii siku inatambua zile jitihada zinazofanywa na mwanamke huyu ili kuzipa thamani” aliongeza.

Akiongelea baadhi ya program zinazowezeshwa na serikali alisema kuwa zipo kwa ajili ya kuwasaidia wanawake kukua kiuchumi. “Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan amewezesha program mbalimbali. Mfano Kizazi cha Usawa, hii inatambua jitihada za wanawake wanazofanya na wanapewa elimu juu ya uzalishaji, masuala ya kilimo, mifugo na kazi za mikono ili kuendeleza uchumi wao na kuleta usawa katika kumiliki mali na ardhi ili mwanamke awe na usawa katika masuala ya kiuchumi” alisema Sichona.

Kwan upande wake mkazi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Hadija Sued alisema kuwa ni mara yake ya kwanza kusikia maadhimisho hayo. Alisema kuwa maadhimisho hayo ni muhimu kwa sababu yatawahamasisha wanawake kuongeza juhudi katika shughuli zao za uzalishaji mali.

Maadhimisho ya Siku ya mwanamke anayeishi kijijini mwaka 2023 yaliongozwa na kaulimbiu isemayo “Wezesha wanawake vijijini kwa uhakika wa chakula; lishe na uendelevu wa chakula”.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.