• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji la Dodoma liwe na vitu bora, maisha bora, DUWASA waanza na maji

Imewekwa tarehe: October 12th, 2020

MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge amesema kuwa ili Jiji la Dodoma liweze kuvutia kwa maendeleo lazima liwe na vitu muhimu pamoja na maisha bora kwa wananchi wake.

Mkuu wa Mkoa alisema hayo katika ziara yake ya kutembelea na kukagua mradi wa maji wa muda mfupi unaotekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mjini Dodoma (DUWASA) wa uchimbaji visima eneo la Ihumwa ikiwa ni mpango wa muda mfupi wa kutatua changamoto ya upatikanaji wa maji jijini hapa.

Dkt. Mahenge aliyataja mambo muhimu yatakayoweza kuleta maendeleo kwa kasi katika Jiji hilo kuwa ni miundombinu safi ya usafirishaji, upatikanaji wa maji, afya na mazingira bora na rafiki katika elimu.

Mkuu huyo wa Mkoa aliishukuru Serikali Kuu kupitia Wizara ya Maji kwa kutenga kiasi cha shilingi bilioni moja na kuipatia Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Mjini Dodoma (DUWASA) kwa ajili ya kutekeleza mradi wa kuchimba visima  kwa muda mfupi ili kutatua kero za upatikanaji maji mjini Dodoma.

“Ili Jiji la Dodoma liweze kuvutia na ni utaratibu wa majiji yote duniani lazima yaweze kuwa na mambo muhimu ikiwemo maisha bora kwa wakazi wa maeneo husika. Hivyo, napenda kuishukulu Serikali Kuu kwa kuimarisha kwa kiasi kikubwa mambo hayo muhimu ambayo ni miundombinu ya usafirishaji, afya, maji, mazingira bora na rafiki ya elimu” alisema Dkt. Mahenge.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu, Wizara ya Maji, Mhandisi Anthony Sanga amesema kuwa kupitia Wizara ya Maji wametoa shilingi billioni moja kwa DUWASA kwa ajili ya kutekeleza mradi wa muda mfupi wa uchimbaji wa visima mjini hapa.

Aliongeza kuwa “Serikali kupitia Wizara ya Maji imeamua kuipatia DUWASA shilingi bilioni moja kwa ajili ya kutekeleza mradi huu wa kuchimba visima katika maeneo mbalimbali ikiwemo hapa Ihumwa. Kutokana na ongezeko la uhitaji wa Maji jijini Dodoma, tumeamua DUWASA watekeleze kwanza mradi huu wa muda mfupi ili kutatua kero za upatikanaji wa maji mjini hapa.

Sisi kama Wizara tunayo miradi ya muda mrefu, tunaendelea kuusanifu kwa kina mradi huo wa kuunganisha mtandao wa Maji kutoka Ziwa Victoria kuja mpaka hapa Dodoma“ alisisitiza Mhandisi Sanga.

Aidha, kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji (DUWASA), Mhandisi David Pallangyo alisema mradi huo wa muda mfupi wa kuchimba visima utatekelezwa katika maeneo kadhaa jijini hapa kwa kuzingatia ongezeko la uhitaji wa maji.

Hata hivyo, Mhandisi huyo ametoa tathimini ya kukamilika kwa mradi huo ambao utatumia muda wa miezi miwili mpaka mitatu kwa kuchimba visima vyenye urefu wa mita 150.

“Sisi kama DUWASA kufuatia kuongezeka kwa uhitaji wa Maji katika maeneo mbalimbali jijini Dodoma tumeona kuja na mradi wa muda mfupi ambao utapuguza changamoto za upatikanaji maji mjini.

Kwa utekelezaji wa kuchimba visima hivi sio kwa eneo hili moja la Ihumwa, bali tutachimba maeneo mbalimbali visima vyenye urefu wa mita 150 ambapo tutatumia muda wa miezi miwili mpaka mitatu“ alisema Mhandisi Pallangyo.

Kwa habari zaidi bofya hapa: DUWASA kutumia Bilioni 2.4 kuchimba visima Dodoma (HabariLeo)

MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge (kushoto) akijadiliana na Katibu Mkuu, Wizara ya Maji, Mhandisi Anthony Sanga (katikati) na Mkurugenzi Mtendaji wa DUWASA Mhandisi David Pallangyo alipotembelea na kukagua mradi wa maji wa muda mfupi unaotekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mjini Dodoma (DUWASA).


MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge (wa pili kulia) akijadiliana kitu na Katibu Mkuu, Wizara ya Maji, Mhandisi Anthony Sanga (wa pili kushoto) wakati zoezi la uchimbaji kisima likiendelea Ihumwa alipotembelea mradi huo wa uchimbaji visima Jijini Dodoma unaoendelea.

Mkurugenzi Mtendaji wa DUWASA Mhandisi David Pallangyo akifafanua kuhusu Mradi wa Muda Mfupi wa Uchimbaji Visima mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani).


Mafundi wakiendelea na kazi ya kuchimba visima.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.