• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji laanza safari kujitegemea, mapato ya ndani kutikisa

Imewekwa tarehe: June 19th, 2019

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imepanga kujenga majengo saba yenye ukubwa tofauti ikiwemo hoteli ya kisasa itakayokuwa na ghorofa 11 na vyumba 117 katika eneo lilipo jengo la ‘Paradise’ kwa sasa,  katikati ya Jiji hilo itakayojulikana kama ‘Dodoma City Hotel’.

Mbali ya hoteli hiyo, Halmashauri hiyo pia itajenga jengo lenye ghorofa pacha jirani na viwanja vya Nyerere litakalojulikana kama ‘Nyerere Square Plaza’ huku Government City Complex’ litakalokuwa na ghorofa sita likijengwa katika eneo la Mtumba ulipo Mji wa Serikali.

Akizungumza wakati wa Baraza Maalum la Madiwani wa Halmashauri hiyo jana Jijini humo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Godwin Kunambi alisema wamepanga kujenga miradi hiyo mikubwa kimkakati na kwa kutumia mapato ya ndani ya Halmashauri ili iwe vyanzo vya kudumu vya Halmshauri hiyo iliyolenga kujitegemea na kujiendesha kwa mapato yake kabla ya mwaka 2025.

Kunambi alisema majengo mengine ni pamoja na ‘Dodoma City Complex’ litakalokuwa na ghorofa nne na litajengwa katika eneo la Dodoma Makulu Barabara ya kuelekea Chuo Kikuu cha Dodoma, ambapo pia kutajengwa jengo jingine la ‘Apartments’ katika eneo hilo.

“Mradi mwingine itakuwa ni ‘Nunge Investment’ ambalo litakuwa jengo la ghorofa 9, huku likiwa na  migahawa mingi ya kisasa ndani yake” alisema Kunambi mbele ya wajumbe wa Baraza hilo lenye Madiwani 60.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo, Halmashauri hiyo itajenga jengo lingine litakaloitwa ‘Dodoma City Plaza’ katika eneo ambapo kuna ukumbi wa ‘NK’ Jijini humo na kufanya Jiji kuwa na majengo saba yatakayotoa huduma mbalimbali kama malazi, vyakula, makazi, Ofisi na kumbi za mikutano.

“Mheshimiwa Mwenyekiti, tuko tayari na tunaanza sasa…tutasaini mikataba ya ujenzi kabla ya Julai 5, 2019 kwa ajili ya majengo mawili ya Dodoma City Hotel na lile la Government City Complex litakalokuwa ndani ya Mji wa Serikali pale Mtumba…haya majengo mawili tunayajenga kwa fedha zetu za mapato ya ndani ya Halmashauri” alisisitiza Kunambi.

Alisema miradi mingine itajengwa kwa kuomba fedha Serikali Kuu kupitia miradi ya kimkakati, na mingine itajengwa kwa Halmashauri kukopa fedha katika mabenki.

Mkurugenzi Kunambi alisema miradi hiyo itakuwa na tija kubwa ikiwemo kuongeza mapato ya Halmashauri, kuongeza ajira kwenye Jamii, kuufanya Mji wa Dodoma kuvutia na kuongeza ujio wa watalii na wageni wengine. Aidha miradi hii itasaidia Jiji kupunguza utegemezi kutoka Serikali Kuu, na kuvutia wawekezaji.

Wajumbe wa Baraza hilo wakiongozwa na Mwenyekiti ambaye ni Mstahiki Meya Prof. Davis Mwamfupe walielezea kuvutiwa na miradi hiyo huku wakishauri ujenzi wake ukamilike kwa wakati ili iwe na tija na kufikia malengo.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.