• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji laendelea kutoa elimu Wiki ya Mazingira

Imewekwa tarehe: June 2nd, 2021

Na Nemes Michael, DODOMA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeendelea kutekeleza kaulimbiu ya wiki ya mazingira duniani isemayo “Tutumie nishati mbadala ili kuongoa mfumo ikolojia”, kwa kutoa elimu ya mazingira na jinsi ya kuyahifadhi katika banda la maonesho kuelekea kilele cha siku ya Mazingira Duniani katika viwanja vya Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete jijini humo.

Akizungumzia maadhimisho hayo yanayoendelea duniani kote, Afisa Mazingira wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Ally Mfinanga alisema kuwa, wamefanikiwa kuungana na wadau mbalimbali wanaohusika katika sekta ya mazingira kuhakikisha wanatoa elimu kwa wakazi wote wa Dodoma na Watanzania kwa ujumla hususan wale watakaotembelea mabanda ya maonesho hayo kwani kuna wataalam mbalimbali wanaotoa elimu ya utunzaji wa mazingira na jinsi ya kukabiliana na athari za tabia ya nchi.

“Tunatumia fursa hii kuhamasisha wakazi wote wa Jiji la Dodoma katika upandaji miti, na ndiyo njia sahihi katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia ya nchi, lakini pia nasisitiza matumizi ya nishati mbadala ili kuweza kuokoa mfumo wa ikolojia” alisema Mfinanga.

Mfinanga aliongeza kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeweka mikakati endelevu katika kuhakikisha maendeleo ya utunzaji wa mazingira na matumizi ya nishati mbadala.

Kwa upande wake, mhasibu wa kikundi cha GRK Group Tanzania ambaye pia ni mjasilimali Pendo Kasogota alisema kuwa kaulimbiu inayotumika inatukumbusha umuhimu wa mazingira katika maisha yetu ya kila siku.

“Kaulimbiu ya wiki ya mazingira inatukumbusha kutambua umuhimu wa mazingira hivyo, yatupasa kuyatunza, kuyapenda na kuyaheshimu mazingira lakini pia maadhimisho haya yanatusaidia wajasiliamali wadogo katika kuonekana hata kufahamika” alisema Kasogota.

Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani yanafanyika kitaifa jijini Dodoma kuanzia tarehe 1 Juni hadi tarehe 5 Juni, 2021 katika viwanja vya Kituo cha Mikutano cha Jakaya Mrisho Kikwete ambapo mgeni rasmi katika ya kilele anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.