• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji lajipanga kuboresha bwawa la Zuzu

Imewekwa tarehe: August 30th, 2021

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imepanga kuendeleza bwawa la Zuzu ili kuwa na tija kwa wakazi wa Jiji hilo kwa kuwahakikishia lishe bora na kuongeza mapato ya ndani.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Idara ya Mifugo na Uvuvi, Gratian Mwesiga alipowasilisha taarifa ya bwawa la Zuzu kwa Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma walipotembelea bwawa hilo.

Mwesiga alisema kuwa kutokana na umuhimu wa bwawa hilo, katika mwaka wa fedha ujao, Halmashauri itashirikiana na wadau na kuangalia mpango wa kuendeleza bwawa hilo.  Aliongeza kuwa bwawa hilo ni muhimu kwa sababu linawawezesha wananchi kupata uhakika wa lishe bora. Bwawa hili likiendelezwa litaiwezesha Halmashauri pia kupata mapato ya ndani.

Akiongelea samaki katika bwawa hilo, Mkuu huyo wa idara alisema samaki waliomo kwenye bwawa hilo waliletwa na maji ya mvua kutoka kwenye mabwawa ya wafugaji wa samaki walio maeneo ya jirani baada ya mabwawa hayo kufurika. “Samaki hawa waliingia kama mayai au vifaranga ambao wameendelea kukua na kuzaliana. Samaki wanaopatikana kwenye bwawa hili ni Kambale na Perege. Mpaka sasa bwawa hili lina jumla ya wavuvi 15. Wavuvi wote hawa wamelipa leseni ya uvuvi kwa mwaka 2021” alisema Mwesiga.

Akiongelea jinsi bwawa hilo lilivyoanza, alisema kuwa lilianza kama mbuga kwa miaka mingi na wakazi wa eneo hilo waliitumia kulima mpunga. “Zamani kwenye mbuga hii kulikuwa na miti mingi hivyo, maji yalikuwa yanatuama na kukauka. Baada ya kukata miti, maji hayakuendelea kutuama kwa muda mrefu, yalijaa wakati wa mvua na baadae kukauka” alisema Mwesiga.

Maji katika bwawa hilo yalianza kujaa tangu mwaka 2018 na yameendelea kuongezeka hadi mwaka 2021 na samaki wameanza kupatikana mwanzoni mwa mwaka huu.

Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Dodoma Meja Mst. Johnick Risasi alisema kuwa kamati yake imefurahia kuona wakazi wa Kata ya Zuzu wakinufaika na bwawa hilo na kuishauri halmashauri kufikiria namna na kuliendeleza bwawa hilo ili liwe na tija zaidi kwa wananchi na kuiwezesha halmashauri kupata mapato.

Nae Katibu wa CCM Wilaya ya Dodoma, Sophia Kibaba alishauri kuwa kina cha bwawa hilo kiongezwe ili kuongeza uhakika wa upatikanaji Samaki.

Bwawa la Zuzu lipo Tarafa ya Zuzu, Kata ya Zuzu likigusa mitaa ya Pinda, Chididimo, Sokoine na Mtaa wa Bihawana katika kata ya Mbabala na Mtaa wa Michese kata Mkonze.

Muonekano wa Bwawa la Zuzu.  

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.