• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji lakabidhi Pikipiki, Vifaa vya usafi vya Milioni 28 kwa Vikundi

Imewekwa tarehe: April 11th, 2019

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma kupitia Mradi wa Uendelezaji Miji ya Kimkakati Tanzania (TSCP) limetoa Pikipiki tatu za Magurudumu Matatu (Toyo) na vifaa vya kutunzia uchafu vyenye thamani ya shilingi Milioni 28.4 kwa vikundi vitatu vinavyofanya kazi za uzoaji taka ngumu kwenye makazi na maeneo ya biashara, ikiwa ni juhudi za kuimarisha usafi na usimamizi wa taka ngumu katika jiji hilo.

Makabidhiano ya pikipiki hizo yamefanywa jana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge kwa vikundi vitatu ambavyo ni Dodoma Youth Environmental Care and Sanitation Group ambacho kinafanya kazi zake katika Kata ya Kizota, Mshikamano Group - Nzuguni C ambacho kinafanya kazi zake katika Kata ya Nzuguni pamoja na Kikundi cha Soft Chivwele Group ambacho kinafanya kazi katika Kata ya Miyuji.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Dkt Mahenge alipongeza juhudi mbalimbali zinazofanywa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi katika kuhakikisha Jiji la Dodoma linakuwa katika Mazingira safi na salama.

“Jambo la kwanza ni kukupongeza Mkurugenzi kwa kazi nzuri unayofanya. Katika karne hii ya 21 majiji ya kisasa ni lazima yaongozwe na usafi na sisi tuna bahati kwamba tumepata fursa hiyo ya kujenga Makao Makuu ya nchi kwenye karne hii ya 21 ambayo imejaa teknolojia za kisasa, kwa hiyo tukitumia vizuri teknolojia tutakuwa na jiji la kisasa kuliko majiji mengine duniani” Alisema Dkt. Mahenge.

Mkuu huyo wa Mkoa alisisitiza vikundi hivyo kuwa wasitumie pikipiki hizo kufanya biashara nyingine tofauti na kazi ya uzoaji taka katika kata mbalimbali za Halmshauri ya Jiji hilo.

Aidha, Dkt. Mahenge alipiga marufuku kufanya shunguli za kilimo na ufugaji katikati ya mji, na kudai kuwa, Jiji katika mipango yake limeainisha maeneo mahsusi kwa ajili ya kufanya kilimo na ufugaji hivyo ni kosa kufanya shughuli hizo katikati ya Mji.

“Dodoma tunayo ardhi ya kutosha kufanya kilimo na ufugaji nje ya eneo la Makao Makuu ya nchi, ufugaji katikati ya mji unaweza kusababisha ajali, kwa hiyo ni marufuku na nimekwisha waagiza viongozi wote wanaohusika” alisisitiza Dkt. Mahenge.

Akizungumza katika tukio hilo, Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi, aliwataka wakazi wa jiji hilo kushirikiana kwa karibu na Halmashauri ili kuhakikisha mazingira yote yanakuwa safi, na kwamba wajenge utamaduni wa kutoa fedha za tozo ya uzoaji taka kwa ajili ya kuviwezesha vikundi hivyo kufanya kazi hiyo ya uondoshaji taka kwa ufanisi mkubwa.

Akiwasilisha changamoto hiyo ya michango kwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Kunambi alisema kuwa, pamoja na juhudi kubwa zinazofanywa na Halmashauri yake katika kuhakikisha mazingira yanakuwa safi, lakini bado kuna baadhi ya wananchi na taasisi hazitoi ushirikiano kwa kutoa tozo za uzoaji taka.

“Napenda Wananchi watambue kuwa, haya magari yanawekwa mafuta, na gharama za uendeshaji wake ni kubwa, hivyo ni lazima wachangie, bado tunachangamoto ya kulipia kwenye kaya na kwenye baadhi ya taasisi…hatuwezi kuwa na mji safi kama wananchi hawachangii. Kwa hiyo, kwa kushirikiana na wenzetu wa ‘Green Waste’ tunawakumbusha wananchi kuchangia zoezi hili kwa sababu kusafisha jiji ni jukumu letu sote” alisema Kunambi.

Hata hivyo, Kunambi alitumia fursa hiyo kutoa elimu kwa wananchi kuwa magonjwa mengi yanatokana na uchafu na hivyo kuwaomba wananchi kushirikiana na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuweka mazingira safi. 

Naye Kaimu Afisa Mazingira wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Ally Mfinanga alivitahadharisha vikundi vyote kuwa pikipiki hizo zinapaswa kuwa katika hali nzuri katika kipindi chote cha matumizi na kuvikumbusha kuwa vitawajibika kulipa kodi stahiki za Serikali zinazohusiana na uendeshaji wa pikipiki za magurudumu matatu.

“Vikundi vyote vitawajibika kulipa kodi, kufuata sheria, kanuni, na taratibu za uendeshaji wa vyombo vya moto na usalama barabarani, na niongeze kwa kusema kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma au mwakilishi wake atakuwa na haki ya kufanya ukaguzi wa mara kwa mara wa pikipiki hizi pasipo kutoa taarifa kwa kikundi husika” alisema Mfinanga.

Alivitaka vikundi vyote kufungua akaunti Benki itakayotumika kuweka fedha za matengenezo ya pikipiki hizo angalau kiasi kisichopungua laki moja na nusu kwa mwezi na risiti ya fedha hizo kuwasilishwa katika Ofisi ya Mkurugenzi.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.