• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Madarasa 44 yaandaliwa kidato cha kwanza

Imewekwa tarehe: February 16th, 2019
  • Halmashauri yatii agizo la Waziri TAMISEMI
  • Bil 1,313,000,000 zatumika kujenga madarasa mapya 37, kukarabati madarasa 7 na ukamilishaji wa maabara katika shule 8
  • Wanafunzi 2,610 waliokosa nafasi waitwa kujiunga na shule
  • Kasi na utekelezaji huu yamkuna Mkuu wa Mkoa wa Dodoma
  • Wananchi, wanafunzi waishukuru serikali ya awamu ya tano
  • Mkurugenzi Kunambi asisitiza kuendelea kuimarisha miundombinu zaidi katika sekta ya elimu

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma ipo katika hatua za mwisho kukamilisha ujenzi wa madarasa mapya 37 na kukarabati madarsa mengine saba huku ukamilishaji wa maabara nao ukiendelea kwa kasi ili madarasa yaliyokua yanatumika kama maabara katika shule nyingi yabaki kwa matumizi ya madarasa.

Mkurugenzi wa jiji Godwin Kunambi amesema hatua za haraka zilichukuliwa na jiji la Dodoma kutokana na upungufu wa madarasa takribani 52 na kupelekea jumla ya wanafunzi 2,610 kukosa nafasi za kujiunga kidato cha kwanza hapa Jijini.

Katika kikao kilichoitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma mwanzoni mwa mwezi huu, Kunambi alibainisha mikakati hiyo ya ujenzi wa madarasa ilivyofanyika kwa haraka ambapo katika kuhakikisha ufanisi na ubora uliokusudiwa unapatikana, alifanya kikao na Wakuu wa Shule wote na kupanga mpango mkakati wa usimamizi wa ukamilishaji wa ujenzi huo.

Aidha Kunambi ameeleza kuwa, kila Mkuu wa Idara wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma alikabidhiwa Shule kwa ajili ya kusimamia ili ujenzi ufanyike kwa haraka na ufanisi ikiwa ni pamoja na kuzingatia taratibu stahiki za ujenzi na manunuzi.

Akielezea siri ya mafanikio hayo ya ujenzi yaliyochukua takribani mwezi mmoja tu, Kunambi alisema amepata ushirikiano kutoka kwa Wakuu wa Shule, Watendaji, na Madiwani, huku akitoa wito kwa wadau wote kuendeleza  mshikamano huo ili kuwaletea maendeleo Wakazi wa Jiji la Dodoma.

"Jiji la Dodoma limekua na ongezeko kubwa la watu kutokana na kuwa na wakazi wengi wanaohamia Dodoma kikazi kwa kuwa Serikali yote inahamia Dodoma kwa sasa, hivyo mahitaji ya miundombinu katika sekta mbalimbali yanaongezeka sana" amefafanua Kunambi.

Maeneo mbalimbali katika Kata zote za Jiji la Dodoma yanaendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali kama ujenzi wa vituo vya afya, ujenzi wa matundu ya vyoo, ujenzi wa maabara, ujenzi wa madarasa, hosteli, nyumba za walimu, ujenzi wa masoko na majengo ya  ofisi za Kata na Ofisi za Shule.

Baadhi ya Kata zilizotembelewa na kukuta miradi mbalimbali ikitekelezwa ni pamoja na Mtumba, Hombolo, Ihumwa, Kikombo, Nzuguni, Ipagala, Dodoma Makulu, Kilimani, Ntyuka, Mkonze, Mpunguzi, Mbabala, Zuzu, Chigongwe, Msalato, Mnadani, Kiwanja cha Ndege, Mbalawala, Nala, Viwandani na Nkuhungu.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.