• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji Dodoma laongeza uwezo kwa kujitegemea, sasa ni asilimia 47

Imewekwa tarehe: September 27th, 2019

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeongeza uwezo wa kujitegemea kwa asilimia 13 kwa mwaka wa fedha 2018/2019 katika jihudi zake za kujitegemea kimapato.

Kauli hiyo ilitolewa na katibu wa Baraza la Madiwani ambaye pia ni Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi alipokuwa akiwasilisha taarifa ya kukamilika kwa ufungaji hesabu za Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2018/2019 kwenye mkutano maalum wa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kupitia hesabu za mwaka wa fedha 2018/2019 katika ukumbi Mikutano wa Halmashauri.

Kunambi alisema kuwa uwezo wa Halmashauri kujitegemea umepanda kwa asilimia 13. “Mheshimiwa Mwenyekiti, hesabu zetu za mwaka 2018/2019 zinaonesha kuwa, uwezo wa kujiendesha kwa kutumia mapato ya ndani umepanda kutoka asilimia 34 ya mwaka uliopita hadi kufikia asilimia 47. Mheshimiwa Mwenyekiti, asilimia ya uwezo wa kujitegemea unakokotolewa kwa kulinganisha jumla ya mapato ya ndani na matumizi yote ya Halmashauri kwa mwaka husika” alisema Kunambi. Matumizi yanayolinganishwa yanajumuisha fedha za mapato ya ndani, ruzuku ya mishahara, miradi ya maendeleo inayofadhiliwa na serikali, wahisani pamoja na matumizi mengineyo, alisema Kunambi.  

Akiongelea uwezo wa Halmashauri kulipa madeni, Kunambi alisema kuwa uwezo wa kulipa madeni kwa mwaka 2018/2019 umeongezeka kutoka uwiano wa 1.5:1 ya mwaka uliopita hadi 2.6:1 mwaka huu, alieleza. “Ukokotoaji wa uwiano hufanyika kwa kuchukua jumla ya thamani ya mali za muda mfupi tulizonazo na kugawanya na jumla ya madeni yote ya muda mfupi” alisema Kunambi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Dodoma mjini, Robert Mwinje amepongeza mkutano huo, na kuutaja kuwa mkutano mzuri. “Kipekee taarifa hii tuliipata mapema na kuipitia. Mimi kitaaluma ni mhasibu, hongera sana mkurugenzi wa jiji kwa taarifa nzuri. Waheshimiwa madiwani hakuna taarifa iliyofichwa” alisema Mwinje. Taarifa inaonesha uwezo wa halmashauri kukua mwaka hadi mwaka, hili ni jambo zuri la kujivunia.

Akichangia hoja katika kikao hicho Diwani wa kata ya Chang’ombe kupitia Chama cha Mapinduzi Mhe. Bakari Fundikira amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kumwamini na kumteua Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kwani amekua chachu ya maendeleo katika Jiji hilo kutokana na ufanisi wake mkubwa katika kazi hasa katika kuiwezesha Halmashauri kujitegemea kutokana na mapato yale ya ndani.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Patrobas Katambi alipongeza kwa uwasilishaji mzuri wa taarifa ya kukamilika kwa ufungaji hesabu za Halmashauri kwa mwaka 2018/2019.

Diwani wa kata ya Chang’ombe kupitia Chama cha Mapinduzi Mhe. Bakari Fundikira akichangia hoja kwenye Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani wa Jiji la Dodoma kupitia taarifa ya kukamilika kwa ufungaji hesabu za Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2018/2019.

Katibu wa Baraza la Madiwani ambaye pia ni Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma akitoa ufafanuzi wakati wa uwasilishaji wa Taarifa ya Hesabu za kufunga mwaka za Halmashauri ya Jiji la Dodoma mbele ya madiwani na wataalam wa jiji la Dodoma (hawapo pichani). Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini Patrobas Katambi na katikati ni Naibu Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma Mhe. Emmanuel Chibago.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.