• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji lapania 'kufuta ziro' kwenye sekondari zake

Imewekwa tarehe: July 26th, 2019

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeweka mkakati wa kuondoa daraja la sifuri 'zero' katika matokeo ya mitihani ya kitaifa kwa wanafunzi wa shule za sekondari.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Idara ya Elimu ya Sekondari katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Martin Nkwabi katika kikao kazi kilichohusisha wataalam wa idara ya elimu sekondari wa Halmashauri ya Jiji, wakuu wa shule zote za sekondari na maafisa elimu Kata; na kufanyika katika ukumbi wa shule ya sekondari ya Dodoma.

Wakati akifungua kikao kazi hicho, Nkwabi alisema kuwa kinalenga kuweka mbinu na mikakati itakayosaidia kuboresha ufundishaji na kuinua zaidi ufaulu kwa shule za sekondari za Halmashauri ya Jiji la Dodoma. "Kama mwaka huu imewezekana kwa shule ya sekondari Dodoma kutokuwa na 'four' au 'zero' basi moto huu tuuendeleze kwenye shule zote za sekondari za Jiji letu, na hilo linawezekana kama kwa pamoja tutachapa kazi" alisema Nkwabi.

Akiongelea suala la upandishaji madaraja kwa walimu, mkuu huyo wa idara ya elimu sekondari alisema kuwa suala hilo linaendelea kushughulikiwa na Halmashauri likiwa katika hatua nzuri ya utekelezaji. Alisema kuwa wakati serikali ikiendelea kufanyia kazi suala la madaraja, walimu wanawajibu wa kutekeleza majukumu yao kwa viwango vya juu ili kufikia malengo ya elimu ya Halmashauri.

Kikao kazi hicho kiliazimia kufuta daraja sifuri kwa shule zote za sekondari katika Halmashauri hiyo na kuanzisha makambi ya kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha Nne. Azimio lingine lilikuwa ni kuinua kiwango cha uwajibikaji kwa walimu wote katika Halmashauri.

Ikumbukwe kuwa katika matokeo ya mtihani wa kumaliza kidato cha sita shule ya sekondari ya Dodoma ilifaulisha kwa kiwango cha daraja la I, II na III tu.

Afisa Elimu Sekondari wa Jiji la Dodoma Martin Nkwambi (mwenye suti nyeusi) akiongoza kikao kazi kupanga mikakati wa kuhakikisha ufaulu unapanda katika jiji la Dodoma. Aliyesimama kulia ni Mkuu wa Shule ya Sekondari Dodoma akiwakaribisha wajumbe wa kikao hicho kilichofanyika tarehe 24/07/2019 katika ukumbi wa mikutano wa Shule ya Sekondari Dodoma.

Watumishi wa Idara ya Sekondari, Maafisa Elimu Kata na Wakuu wa Shule za Sekondari za Jiji la Dodoma wakishiriki kikao kazi cha kuweka mkakati wa kuboresha elimu na kuinua ufaulu kwa shule za sekondari za Jiji la Dodoma.

Watumishi wa Idara ya Sekondari, Maafisa Elimu Kata na Wakuu wa Shule za Sekondari za Jiji la Dodoma wakishiriki kikao kazi cha kuweka mkakati wa kuboresha elimu na kuinua ufaulu kwa shule za sekondari za Jiji la Dodoma.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Viwanjani Kaizirege Adelifi akichangia mada wakati wa kikao kazi cha kuweka mkakati wa kuboresha elimu na kuinua ufaulu kwa shule za sekondari za Jiji la Dodoma.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.