• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji lapokea vifaa tiba kutoka PSSSF

Imewekwa tarehe: June 24th, 2021

Na Noelina Kimolo, DODOMA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeushukuru Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kwa msaada wa vifaa tiba katika kitengo cha akina mama wajawazito na kitengo cha meno kwa lengo la kuboresha huduma katika Kituo cha Afya Makole vilivyotolewa na mfuko huo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka huu.

Shukrani hizo zimetolewa na Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo Dkt. Andrew Method kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Joseph Mafuru wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya vifaa hivyo iliyofanyika katika kituo hicho leo Juni 24, 2021.

Mganga Mkuu huyo alisema kuwa, vifaa hivyo vina umuhimu mkubwa katika kuendeleza na kuboresha huduma kwenye upande wa akina mama wajawazito hususani wale wanaohitaji upasuaji na meno.

“Tumepata dawa nyingi ambazo zinahitajika katika upasuaji pamoja na nyuzi, lakini pia tumepata dawa na vifaa ambavyo vitatusaidia katika upande wa meno” alisema Dkt. Method.

Dkt. Method alisema kituo hicho ni moja ya vituo ambavyo vinahudumia wananchi wengi hususan baada ya Serikali kuhamia Dodoma hivyo, wanaamini kwa msaada huo uliotolewa na PSSSF wananchi wengi watanufaika nao katika kupata matibabu.

Aidha, Dkt. Method alimpongeza Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Mhe. Antony Mavunde kwa ushirikiano mkubwa anaouonesha kwa kuwatafuta wadau mbalimbali wa maendeleo wanaosaidia kuboresha huduma za afya katika Jiji la Dodoma.

Akikabidhi vifaa hivyo, Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF Hosea Kashimba alisema kuwa, taasisi anayoiongoza inatambua kazi kubwa inayofanywa na Kituo cha Afya Makole katika kutoa huduma za afya kwa wakazi wa Jiji wakiwemo watumishi wa mfuko huo.

“Kwa kuzingatia ujirani wetu huu, PSSSF imekuwa ikitoa misaada mbalimbali kwa kituo hiki ikilenga kuboresha huduma zitolewazo kwani kama mjuavyo nia ya Serikali ni kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za afya na ili kuhakikisha tunaendeleza nia hiyo, katika maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka huu tunachangia vifaa tiba katika kitengo cha akina mama wajawazito na kitengo cha meno kwa lengo la kuboresha utoaji wa huduma za tiba ya meno ikiwemo utengenezaji wa meno bandia” alisema Kashimba.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Mhe. Antony Mavunde ambaye ndiye aliyepokea vifaa hivyo alitoa shukrani kwa (PSSSF) kwa niaba ya wananchi wa jimbo lake huku akitoa wito kwa wadau wengine kuiga mfano huo wa PSSSF kusaidia huduma za afya katika Jiji la Dodoma.

“Katika kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka huu, tunatoa shukrani zetu kwa PSSSF kwa kutuletea msaada kwenye kituo hiki” alisema Mavunde kwa unyenyekevu. Aidha, Mhe. Mavunde alisema ushirikiano huo ni mzuri katika kutatua shida mbalimbali za wananchi pamoja na kuleta maendeleo katika katika Jiji la Dodoma na Taifa kwa ujumla.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.