• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji latambua wazee wote, lawapatia vitambulisho

Imewekwa tarehe: July 5th, 2019

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imekamilisha zoezi la kutambua wazee katika Kata zote 41 za Jiji hilo, ambapo jumla ya wazee 19,543 wametambuliwa ikiwa ni utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Wazee ya mwaka 2003 inayolenga kuwaenzi kwa mchango wao katika Taifa kwenye nyanja mbalimbali ikiweno uchumi, siasa, kijamii na kiutamaduni.

Halmashuri hiyo pia tayari imewapatia vitambulisho wazee 10,290 ambavyo vitawatambulisha katika maeneo mbalimbali ya huduma ikiwemo kwenye vituo vya Afya, huku wengine  2,686 vitambulisho vyao vikiwa katika maandalizi.

Hayo yamebainishwa na Afisa Ustawi wa Jamii wa Jiji la Dodoma Rebeka Ndaki wakati akisoma taarifa ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwenye mkutano wa uzinduzi wa Baraza la Wazee Wilaya ya Dodoma jana katika ukumbi Halmashauri ya Jiji, mbele ya mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Patrobas Katambi.

Alisema mpaka sasa Halmashauri ya Jiji  kupitia Idara ya Afya imewafikia wazee katika Kata 33 kati ya 41 za Jiji hilo na kuwapiga picha wazee wapatao 12,979 sawa na asilimia 66.41 ya wazee wote waliotambuliwa ambapo tayari wazee 10,290 wameshapatiwa vitambulisho.

“Halmashauri ya Jiji katika kipindi cha kuanzia Mwezi Julai 2018 hadi Juni 2019 imetekeleza maelekezo ya Serikali ya kutoa huduma ya matatibu bure kwa wazee ambapo jumla ya wazee 4,551 walihudumiwa katika vituo vya huduma vya Jiji wakitumia vitambulisho vya wazee” ilisema sehemu ya taarifa ya Halmashauri hiyo.

Akizungumza na wazee hao kabla ya kuzindua rasmi Baraza hilo, Mkuu wa Wilaya Katambi alitoa wito kwa jamii nzima kuwajali na kuwaenzi wazee kwani wamefanya kazi kubwa katika ujenzi wa Taifa na kuweka mazingira rafiki  kwa vijana wa sasa kuishi kwa amani na utulivu.

“Wazee ni tunu ya Taifa, juhudi zao za muda mrefu ndiyo zimetufikisha hapa kama Taifa kwahiyo ni lazima tuwaenzi kwa kila namna na mimi Ofisi yangu iko wazi wakati wote kwa ajili ya kuwahudumia na kusikiliza changamoto zao” alisema Katambi.

Mkuu wa Wilaya huyo aliitaka jamii hasa vijana kuacha dhana potofu kuwa wazee wamepitwa na wakati, kwani kwa uhalisia vijana ndiyo waliopitwa na wakati kwa kuwa wazee walikuwepo tangu zamani na sasa wapo tofauti na vijana ambao wa kizazi kipya.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.