• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji latoa vibali vya ujenzi zaidi ya 7,100

Imewekwa tarehe: October 5th, 2020

Halmashauri ya Jiji la Dodoma imetoa jumla ya vibali vya ujenzi 7,133 katika kipindi cha miaka mitatu katika kudhibiti ujenzi holela.

Kauli hiyo imetolewa na Afisa Mipango Miji wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Aisha Masanja alipokuwa akiwasilisha mada juu ya uboreshaji wa makazi ndani ya Jiji la Dodoma katika maadhimisho ya siku ya makazi duniani yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu jijini Dodoma.

Masanja alisema kuwa Halmashauri imekuwa ikipokea maombi ya vibali vya ujenzi kwa kasi kubwa tangu Halmashauri hiyo kutangazwa kuwa Jiji. “Katika kipindi cha kuanzia mwezi Julai, 2017 hadi Juni, 2020 jumla ya vibali vya ujenzi 7,133 vimetolewa” alisema Masanja. Vibali vya ujenzi hutolewa ndani ya siku saba kwa maombi ambayo hayana shida, aliongeza.

Akiongelea athari za uendelezaji ujenzi usiozingatia kanuni, taratibu na sheria za mipango miji, Afisa Mipango Miji huyo alisema kuwa unasababisha jiji kukua bila kufuata taratibu zilizopo. Alisema kuwa ukiukwaji wa taratibu hizo hupelekea ujenzi wa majengo yasiyo na mpangilio. Athari nyingine aliitaja kuwa ni kukosekana kwa maeneo ya huduma za kijamii na miundombinu muhimu, hivyo kufikika  kwa shida wakati wa majanga.

Afisa huyo aliongeza athari nyingine ni kupata hasara pindi hatua stahiki za mipango miji zitakapochukuliwa kama ubomoaji ili kupisha miundombinu muhimu. “Ndugu washiriki, athari nyingine ni kukosekana kwa mvuto wa ujenzi” aliongeza Masanja.

Afisa Mipango Miji huyo alisema kuwa katika kufanikisha udhibiti ujenzi holela, Watendaji wa Kata na Mitaa wanawajibu wa kuhakikisha hakuna uvamizi kwenye maeneo ya wazi, hifadhi za barabara na maeneo ya taasisi. “Watendaji wanawajibu wa kuhakikisha wanapata nakala ya mabadiliko ya matumizi ya ardhi au mgawanyo wa kiwanja kwa wananchi watakaoweka mabango katika maeneo yao. Pia, wanawajibu wa kutoa taarifa Halmashauri kama kuna ujenzi wowote usiokuwa na kibali katika maeneo yao” alisema Masanja.

Watendaji Kata na Mitaa wanawajibu wa kukagua ujenzi unaofanyika katika maeneo yao kwa kuhakikisha kuwa wana vibali vya ujenzi. “Halmashauri ya Jiji tumeanzisha matumizi ya rangi ya kupaua au kupakwa katika mapaa ya majengo kwa kata zote 41 za jiji la Dodoma. Katika kutekeleza lengo hili, watendaji wanatakiwa kuhakikisha watu wanajenga na kuezeka kwa kufuata rangi za bati zilizopangwa katika Kata zao” alisisitiza Masanja.

Maadhimisho ya siku ya makazi duniani yaliongozwa na kaulimbiu isemayo “Nyumba bora kwa wote; kwa ukuaji bora wa miji”.

Afisa Mipango Miji wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Aisha Masanja alipokuwa akitoa mada uu ya uboreshaji wa makazi ndani ya Jiji la Dodoma kwenye kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Makazi Duniani kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Jijini Dodoma leo 05 Octoba, 2020.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.