• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji lavuka tena lengo la makusanyo ya ndani

Imewekwa tarehe: August 5th, 2019

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imefanikiwa kukusanya shilingi 71,921,804,660 sawa na asilimia 107.1 na kwa mara nyingine kuvuka lengo la makusanyo ya ndani ya Halmashauri hiyo safari hii kwa asilimia 7.1.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi alipokuwa aliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za serikali kwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa mwaka wa fedha 2018/2019 katika mkutano wa mwaka wa Baraza la Madiwani lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

Kunambi alisema kuwa kwa mwaka wa fedha 2018/2019 bajeti ya makusanyo ya ndani ilikuwa shilingi 67,149,647,027. Halmashauri hiyo ilikusanya shilingi 71,921,804,660 sawa na asilimia 107.1 na kuvuka lengo la makusanyo ya mapato ya ndani kwa asilimia 7.1.

Akiongelea ongezeko la bajeti ya Halmashauri, alisema kuwa bajeti iliongezeka kutoka shilingi 20,798,303,295 mwaka wa fedha 2017/2018 hadi kufikia shilingi 67,149,647,027 mwaka wa fedha 2018/2019 ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 69.02.

Kuhusu mapato halisi ya ndani, yameongezeka kutoka shilingi 25,058,290,451 kwa mwaka wa fedha 2017/2018 hadi kufikia shilingi 71,921,804,660 kwa mwaka wa fedha 2018/2019. Ongezeko hilo ni sawa na asilimia 65.15, aliongeza.

Akifafanua zaidi kuhusu bajeti ya mwaka wa fedha 2018/2019, Mkurugenzi huyo alisema kuwa Halmashauri ilikisia kukusanya na kupokea jumla ya shilingi 159,467,035,337 bila bakaa ya mwaka wa fedha 2017/2018. Fedha kutoka vyanzo vya ndani shilingi 67,149,647,027, ruzuku ya mishahara shilingi 44,599,110,165, ruzuku ya matumizi mengineyo shilingi 6,924,823,507 na ruzuku ya miradi ya maendeleo shilingi 40,793,454,638.

Katika mapato, alisema kuwa kwa mwaka wa fedha 2018/19 Halmashauri ilifanikiwa kupokea jumla ya shilingi 168,446,315,814. Kati ya fedha hizo, shilingi 71,921,804,660 ni vyanza vya ndani vya Halmashauri, shilingi 45,279,048,720 ni ruzuku ya mishahara, shilingi 2,478,129,023 ni ruzuku ya matumizi mengineyo na shilingi 48,767,333,411 ni ruzuku ya miradi ya maendeleo.

Ikumbukwe kuwa kwa mujibu wa ripoti ya ukaguzi kutoka kwa Mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali Halmashauri ya Jiji la Dodoma imepata hati safi kwa miaka miwili mfululizo mwaka 2016/2017 na 2017/2018.



Matangazo

  • TANGAZO LA MABADILIKO YA TAREHE YA USAHILI October 03, 2025
  • TANGAZO LA MAJINA YA WASIMAMIZI JIMBO LA MTUMBA October 03, 2025
  • MAJINA YA WASIMAMIZI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA- DODOMA MJINI October 03, 2025
  • TANGAZO LA MAJINA YA MAKARANI WAOGOZAJI WAPIGA KURA October 03, 2025
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Rc Senyamule awasihi wawekezaji sekta binafsi kuwekeza Dodoma

    October 03, 2025
  • CCTV kamera mwarobaini wa wavunjifu wa sheria jiji la Dodoma

    October 02, 2025
  • Wadau wa afya wapongezwa kwa juhudi zakudhibiti vifo vya wajawazito

    October 01, 2025
  • UONGOZI WA KLABU YA MICHEZO OFISI YA MKUU WA MKOA WA DODOMA WAKUTANA NA RAS KAZUNGU

    September 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.