• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji mnafanya vizuri ujenzi wa miundombinu, sasa jipangeni kuiendesha kwa faida - Dkt. Mahenge

Imewekwa tarehe: August 31st, 2019

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imetakiwa kujipanga katika uendeshaji wa miradi ya kimkakati inayotekelezwa ili isimamiwe vizuri pasipo kuathiri jukumu lake la msingi la utoaji huduma kwa wananchi.

Kauli hiyo alitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge alipofanya ziara ya kawaida ya kutembelea na kukagua miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma jana.

Dkt. Mahenge alisema “nimejiridhisha na utekelezaji wa miradi yote mitatu inaenda vizuri sana. Mkandarasi Mohammedi Builders unafanya kazi nzuri. Pongezi kwa Mkurugenzi wa Jiji na Mkuu wa Wilaya kwa kazi nzuri ya usimamizi”. Aliongeza kuwa uwekezaji huo mkubwa unatarajiwa kukamilisha tarehe 31 Disemba, 2019, na kuitaka Halmashauri kuanza kujipanga itakavyosimamia miradi hiyo na kuifanya kuwa endelevu.

Mkuu wa Mkoa alishauri kuwa baada ya taratibu za uendeshaji wa miradi hiyo kukamilika, mwezi Novemba, 2019 miradi hiyo ianze kutangazwa ili wananchi wa Dodoma na maeneo mengine waanze maandalizi ya uwekezaji katika miradi hiyo. Vilevile, alivikaribisha vikundi mbalimbali, vyuo, shule na wajasiriamali kutembelea maeneo hayo kujionea uwekezaji huo mkubwa na fursa za wao kuwa sehemu ya uwekezaji.

Akiongelea ujenzi unaofanywa na kampuni ya Mohammedi Builders, mkuu wa mkoa alisema anaridhishwa na kazi inayofanywa na mkandarasi huyo. “Mkandarasi Mohammedi Builders unafanya kazi nzuri. Kujenga miradi mitatu kwa pamoja na yote inakwenda vizuri siyo jambo dogo. Nimeridhishwa miradi yote mitatu inakwenda vizuri” alisema Dkt. Mahenge.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi aliitaja ziara ya Mkuu wa Mkoa kuwa ni kujionea kazi inayofanywa na Rais, Dkt. John Magufuli jijini Dodoma. “Serikali imeleta fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji miradi mbalimbali jijini Dodoma. Miradi yote ina hadhi ya Makao Makuu na itakuwa na faida kubwa kwa wakazi wa Dodoma” alisema Kunambi.  

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma alifanya ziara ya kawaida kutembelea na kukagua miradi ya kimkakati ya uboreshaji wa mandhari ya eneo la kupumzikia (Recreational park) katika eneo la Chinangali, ujenzi wa kituo kikuu cha mabasi na soko kuu katika eneo la Nzuguni inayotekelezwa na Jiji la Dodoma.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.