• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji Mwanza walipongeza Jiji Dodoma Uendeshaji wa dampo

Imewekwa tarehe: July 11th, 2019

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imepongezwa kwa ujenzi na uendeshaji wa jalala la kisasa 'dampo' la Chidaya katika jitihada zake za kuhakikisha usafi wa Jiji unaimarishwa na kulinda afya za wananchi.

Kauli hiyo ilitolewa na kiongozi wa timu ya wataalam kutoka Halmashauri ya Jiji la Mwanza Mhandisi Henry Mbaga walipotembelea Halmashauri ya Jiji la Dodoma kujifunza juu ya ujenzi na uendeshaji wa jalala la kisasa Chidaya.

Mbaga alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma imefanikiwa katika ujenzi na uendeshaji wa jalala la kisasa Chidaya. “Timu ya wataalam kutoka Halmashauri ya Jiji la Mwanza imetembelea Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa ajili ya kujifunza jinsi wenzetu walivyofanikiwa katika ujenzi na uendeshaji wa jalala la kisasa. Tunataka kujifunza pia kupitia changamoto ambazo wenzetu wa Dodoma wanakutana nazo na kufanikiwa katika uendeshaji na kubadilishana uzoefu ili tunapoanza kujenga tujenge kwa ufanisi” alisema Mhandisi Mbaga.

Mhandisi huyo alisema kuwa timu yake imejifunza kuwa ushirikishaji wa wadau wanaotekeleza usafi wa mazingira ni jambo la msingi. “Ushirikishaji wa wadau wa usafi wa mazingira ni muhimu, tumeona kuwa mdau anatekeleza majukumu yake ipasavyo na kuwa Halmashauri ndiyo inaratibu. Lakini pia kuhakikisha fedha zinapatikana kwa wakati ili kutokwamisha shughuli za usafi” alisema Mhandisi Mbaga. Vilevile, wamejifunza kuwa uangalizi na matengenezo ya mitambo kwa muda muafaka kunaliwezesha dampo kudumu na kufanya kazi au kutumika kwa muda mrefu.

Katika kutembelea jalala la Chidaya, angalizo lilikuwa wakati wa ujenzi mabomba ya kutolea maji machafu yalindwe ili yaweze kupita vizuri na kuepuka magari kutitia wakati wa mvua. Utaratibu huo utasaidia kuzuia maji yatokanayo na taka kuzuiwa kutokwenda kwenye maeneo husika, aliongeza.

Kwa upande wake, msimamizi wa jalala la kisasa la Chidaya, Godfrey Ngowi alisema kuwa mafanikio katika uendeshaji wa jalala hilo yanatokana na ushirikiano baina ya idara mbalimbali za Halmashauri na wadau. “Ushirikiano huu umekuwa ukiwezesha mahitaji kama mafuta, vilainishi vya mitambo, matengenezo ya mitambo kupatikana kwa wakati” alisema Ngowi.

Mtambo wa kusambaza taka ngumu ukifanya kazi katika dampo la kisasa la Chidaya

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.