• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wakazi wa Jiji watakiwa kujiunga CHF

Imewekwa tarehe: July 10th, 2019

WANANCHI wa mtaa wa Mahomanyika jijini Dodoma wametakiwa kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa (improved Community Health Fund - iCHF)  ili waweze kutibiwa bure mwaka mzima.

Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Sharifa Nabalang’anya alipokuwa akihamasisha wananchi wa mtaa wa Mahomanyika, kata ya Nzuguni jijini hapa katika uzinduzi wa kampeni ya uhamasishaji mkubwa wa wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii Ulioboreshwa uliofanyika katika ofisi ya mtaa huo.

Nabalang’anya alisema kuwa ugonjwa haupigi hodi, hivyo wananchi wanatakiwa kujiandaa kukabiliana na ugonjwa kwa kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii Ulioboreshwa. “Ndugu zangu, CHF iliyoboreshwa ni muhimu. Mheshimiwa diwani, napenda kuonesha masikitiko yangu kwa idadi ndogo ya wananchi waliojiunga na CHF” alisema Nabalang’anya kwa masikitiko.

“Shukrani kwa Rais, Dkt. John Magufuli kwa kuendelea kuongeza bajeti ya Wizara ya Afya kila mwaka. Haya ni mapenzi makubwa ya Rais wetu kwa wananchi. Tumuunge mkono anatuhurumia wananchi. Ombi langu tujiunge na mfuko wa bima ya afya ili tutibiwe mwaka mzima” alisema Nyabalang’anya. Katika kuonesha nia njema ya serikali kwa wananchi wake, kaya moja ikichangia shilingi 30,000 watu sita katika kaya hiyo wanahudumiwa mwaka mzima na serikali inaongezea shilingi 30,000 aliongeza.

Awali mratibu wa CHF katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Patrick Sebyiga alisema kuwa lengo la maboresho ya CHF ni kuhakikisha kuwa wananchi wengi wanajiunga na mfuko huo ambao utawasaidia kupata huduma za afya kwa gharama nafuu.

Mratibu huyo alisema kuwa dhumuni la kuboresha CHF ni kutenganisha watoa huduma za tiba na usimamizi wa bima, kuweka mfumo wa bima, kuongeza idadi ya wananchama, kutoa mfumo wa utambulisho utakaowezesha huduma kupatikana kwa mwanachama akiwa sehemu yeyote katika Mkoa wa Dodoma.  

CHF iliyoboreshwa imebuniwa na wataalam wa mradi wa HPSS- Tuimarishe afya ikiwa imetumia uzoefu wa mifuko ya bima ya afya ya jamii kutoka India pamoja na matokeo ya tafiti zilizofanywa ndani na nje ya nchi.  

Wananchi walioshiriki kampeni ya kuhamasisha wananchi kujiunga na CHF iliyoboreshwa wakisikiliza kwa makini, viongozi wakiongea faida za kujiunga na CHF iliyoboreshwa.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.