• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jjiji lauza viwanja 31 kwa mnada

Imewekwa tarehe: September 28th, 2019

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeingiza viwanja 31 vya kimkakati sokoni kwa njia ya mnada ili kuweka uwazi katika zoezi la uuzaji viwanja hivyo na kuepuka mianya ya rushwa.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano na Uhusiano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo muda mfupi kabla ya kuanza zoezi la uuzaji viwanja kwa njia ya mnada katika eneo la wazi la Manispaa ya zamani jijini hapa.

Fungo alisema “viwanja vinavyouzwa leo vipo 31, ukitaka kuviuza kwa utaratibu wa kawaida utaleta taharuki na mtafaruku mkubwa katika jamii”. Viwanja vyote vitakavyouzwa hapa vipo eneo la Nzuguni, ambalo ni eneo la kimkakati lenye mvuto wa kibiashara katika kitovu cha jiji la Dodoma, aliongeza.  

Alisema kuwa uuzaji wa viwanja hivyo kwa njia ya mnada unaongeza uwazi na uwajibikaji kwa zoezi hilo. “Hapa hakuna mwanya wa rushwa katika zoezi hili. Nikuhakikishie hakuna mtu aliyekuja hapa akijua bei ya kianzio kwa kila kiwanja. Uzuri wa mnada, mtu anajipangia bei mwenyewe” alisisitiza Fungo. Zoezi hili litaondoa malalamiko ya kupendelea mtu au makundi katika jamii. Kupitia mnada huu, Halmashauri nayo itapata mapato yake kwa njia ya uwazi, alisisitiza Fungo.

Mshiriki katika mnada huo aliyejitambulisha kwa jina na Yusta Mushi, kutoka mkoani Arusha alipongeza uamuzi wa kuuza viwanja hivyo kwa njia ya mnada. “Niwashauri tu wasimamizi wa zoezi hili kuwa wakati mwingine waongeze wigo wa matangazo kwa muda wa kutosha kwenye vyombo vya habari ili watu wengi wapate fursa na muda wa kushiriki katika mnada kama huu. Mimi nimekuja jana jioni hivyo kuchelewa zoezi la kwenda kutembelea maeneo ya viwanja vinavyouzwa” alisema Mushi.

Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeingiza sokoni viwanja 31 vya matumizi ya taasisi (1), kituo cha mafuta (1), hoteli (20), maduka makubwa (2), na biashara (7) kwa ajili ya mnada ambavyo vimenadiwa na watu wenye maadili yasiyo na shaka katika jamii. Viwanja hivyo vipo eneo la Nzuguni unapojengwa uwanja wa Taifa, stendi kuu ya kisasa ya mabasi na soko kuu la kisasa. Pia vipo umbali wa Kilomita 7 kutoka katikati ya Jiji la Dodoma na Kilomita 10 kutoka Mji wa Serikali - Mtumba.

Aidha, viwanja hivi vipo karibu na eneo la viwanja vya uwekezaji Njedengwa, na jirani na eneo ambalo litajengwa stesheni ya treni. Pia eneo hili lipo mkabala na uwanja wa sasa wa maonesho ya Kilimo na Mifugo maarufu uwanja wa Nanenane.

Maafisa wa Jiji la Dodoma walioendesha mnada wa uuzaji wa viwanja, pichani ni Alfred Mlowe - Mweka Hazina wa Jiji (kulia), Joseph Fungo - Afisa TEHAMA na Uhusiano wa Jiji (kushoto), Mtalemwa - Afisa Ardhi (wa pili kutoka kushoto) na Aisha Masanja - Afisa Mipango miji.


Chini: Baadhi ya wananchi walioshiriki katika mnada wa uuzaji viwanja 31 vinavyozunguka Soko kuu jipya na Stendi Kuu mpya eneo la Nzuguni Jijini Dodoma.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.