• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

JKT yajizatiti kuunga mkono juhudi ya Serikali katika kilimo

Imewekwa tarehe: October 17th, 2020

MKUU wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Venance Mabeyo (pichani) ameweka jiwe la msingi katika mradi ujenzi wa skimu ya umwagiliaji katika kikosi cha 837 Chita JKT wilayani Kilombero, mkoani Morogoro ukitarajiwa kufanikisha uhakika wa chakula kwa vikosi vya jeshi hilo na taifa kwa jumla.

Lengo la ujenzi wa skimu hiyo ni kuwa na kilimo cha mpunga chenye tija kwa kulima ekari 24,000 kwa misimu miwili ya mwaka ifikapo mwaka 2025. Kwa sasa kikosi hicho kinalima ekari 1,000 kwa mwaka.

Jenerali Mabeyo pia aliweka jiwe la msingi katika ujenzi wa kiwanda cha kuchakata mpunga na kuzindua msimu mpya wa kilimo huku akitaka JKT kuzalisha kwa tija kuondoa hali ya kutegemea chakula cha msaada nchi inapokuwa na upungufu.

Alisema mkakati wa kilimo unaendelea kutekelezwa na JKT ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za serikali ya kutaka kuzalisha kwa tija na kuwa na uhakika wa chakula salama na kutekeleza uchumi wa viwanda.

“Tulizoea tukiwa na njaa tunaagiza chakula kutoka nje, tulizoea kuwatumia wafanyabiasha kutuletea chakula lakini vilevile tulizoea wakati wa njaa kupata chakula cha msaada, nadhani tunahitaji sasa kufika mwisho.

“Na sisi tunataka tuwe sehemu ya kutoa chakula kwa wanaohitaji ndani na nje ya nchi, kwa eneo hili la Chita hilo linawezekana kwa sababu ya kutekeleza kilimo mkakati,” alisema.

Alisema anaamini uwekaji jiwe la msingi katika ujenzi wa skimu ya umwagiliaji ni kiashiria cha uzalishaji wenye tija kwa historia ya kilimo cha umwagiliaji ndani ya JKT.

Mradi wa ujenzi wa miundombinu ya skimu ya umwagiliaji unatarajiwa kukamilika Juni mwakani na itakuwa ikifanya kazi asilimia 100. “Ni mapinduzi makubwa ndani ya JKT na ni imani mradi utakamilika kama ulivyopangwa,” alisema.

Alisema hadi sasa sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi inachangia kwa asilimia 65 ya malighafi ya viwandani nchini hivyo uwezeshaji huo mkubwa wa kilimo cha umwagiliaji, utaongeza malighafi na kupunguza fedha za kigeni zinazotumika kununulia malighafi nje ya nchi Jenerali Mabeyo alitoa Sh milioni 200 kusaidia kukamilisha miundombinu ya skimu ya umwagiliaji na kusisitiza kilimo kitakapoanza kisisimame.

Wakati huo huo aliwataka vijana wa kujitolea kufanya kazi kwa weledi bila kukata tamaa kwani manufaa makubwa yatapatikana kwao. Alitaka JKT kuhakikisha inaangalia uwezekano wa kuongeza wigo wa mazao hususani yanayotoa mafuta kama vile alizeti.

“ Ukilinganisha uzalishaji wa mafuta ya kupikia na mahitaji yetu tuna upungufu wa tani 220,000 hadi tani 340,000 na mwaka 2019 /2020 nchi yetu imetumia kiasi cha Sh bilioni 413 kwa ajili ya kuagiza mafuta,” alisema.

Alisisitiza: “Ni wajibu wetu sasa kuigeuza kuwa fursa kwa kuwekeza katika kilimo cha mazao yanayozalisha mafuta ya kula ili kiasi cha fedha Sh bilioni 413 kinachotumika kuagiza mafuta nje ya nchi kibaki JKT

Chanzo:HabariLeo



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.