• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

JPM apokea ripoti ya CAG na TAKUKURU

Imewekwa tarehe: March 26th, 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo amepokea ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka 2018/19 na ripoti ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ya mwaka 2018/19, Ikulu Chamwino, Mkoani Dodoma.

Katika hafla ya upokeaji wa ripoti hizo, Mhe, Rais Magufuli amempongeza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Charles Kichere kwa kazi nzuri ya ukaguzi ambayo imeonesha maeneo mbalimbali ambayo Serikali imefanya vizuri na maeneo ambayo yanahitaji kufanyiwa kazi, na amewaagiza Makamu wa Rais, Waziri Mkuu na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi kufanyia kazi dosari zote zilizojitokeza katika utendaji kazi wa Serikali.

Vilevile, Mhe. Rais ameipongeza ofisi ya CAG kwa kuanza kukagua mashirika ya umma badala ya kutumia taasisi za ukaguzi za nje hatua hiyo imeokoa shilingi Bilioni 1.4, ikiwa ni pamoja na kuonesha dosari za matumizi ya fedha katika taasisi mbalimbali ikiwemo vyama vya siasa na Jeshi la Polisi.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amempongeza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU ambaye alikuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu, Brig. Jen. John Mbungo kwa kazi nzuri inayofanywa na taasisi hiyo katika kudhibiti vitendo vya rushwa, kuokoa fedha na mali za umma zilizokuwa zimepotea, na pia kurejesha shilingi Bilioni 8.8 za wakulima zilizokuwa zimeibwa kupitia vyama vya ushirika vya wakulima hapa nchini.

Kutokana na kazi hiyo nzuri, Mhe. Rais Magufuli amemteua Brig. Jen. John Mbungo kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU kuanzia leo tarehe 26 Machi, 2020.

Mhe. Rais Magufuli ameelezea kutofurahishwa kwake na viongozi wa Mikoa na Wilaya kutochukua hatua kwa wakati pale wananchi wanapodhulumiwa haki zao, na kwamba haikuwa sawa kwa wakulima kudhulumiwa shilingi Bilioni 8.8 ambazo zimesubiri timu ya TAKUKURU ya kitaifa kuchukua hatua.

Akizungumzia kuhusu maambukizi ya Virus vya Corona amesema hayawezi kuifanya serikali iache kuendelea na vikao vyake vya muhimu ikiwemo vikao vya baraza la madiwani na kutolea mfano Bunge la Jamhuri ya Muungano, na amechukua nafasi hiyo kusisitiza kuwa suala uchaguzi nalo liko pale pale.

Nae, CAG Bw. Charles Kichere amesema ripoti za ukaguzi 19 alizoziwasilisha ni za Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, Mashirika ya Umma, miradi ya maendeleo, ukaguzi wa ufanisi, ukaguzi wa mifumo ya TEHAMA, ufuatiliaji wa mapandekezo yaliyotolewa katika ripoti za ukaguzi wa ufanisi kwa miaka iliyopita na ripoti 12 za ukaguzi wa ufanisi zinazohusu sekta mbalimbali.

Kwa upande wake Brig. Jen. Mbungo amesema utafiti uliofanywa kwa mwaka 2018/19 umeonesha kuwa idadi ya Watanzania wanaoamini kuwa vitendo vya rushwa vimepungua imeongezeka kutoka asilimia 37 (2015) hadi kufikia asilimia 71 na pia ripoti ya Jukwaa la Uchumi Duniani (World Economic Forum – WEF) kwa kushirikiana na sekta binafsi imeonesha kuwa Tanzania imeshika nafasi ya 28 kati ya nchi 136 kwa ufanisi katika matumizi mazuri ya fedha za umma.

Rais Magufuli akipokea Ripoti ya Mwaka 2018-2019 kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi  wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) Brigedia Jenerali John Mbungo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Magufuli akizungumza na viongozi mbalimbali wa Serikali mara baada ya kupokea taarifa ya CAG na TAKUKURU.

Chanzo: globalpublishers.co.tz

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.