• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

JPM apongeza miradi ya Jiji Dodoma

Imewekwa tarehe: November 22nd, 2019

SERIKALI imedhamiria kulijenga Jiji la Dodoma ili liwe la kisasa baada ya kuyapokea Makao Makuu ya nchi.

Kauli hiyo imetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli alipokuwa akiongea na mamia ya wananchi wa Dodoma katika viunga vya stendi kuu ya mabasi inayojengwa eneo za Nzuguni jijini Dodoma leo.

Rais Dkt. Magufuli amesema “tunataka Jiji la Dodoma liwe la mfano. Miradi inayotekelezwa hapa Jiji la Dodoma ikikamilika, Jiji hili litakuwa la kisasa”. Stendi inayojengwa inatarajiwa kuunganishwa na Treni maalum. Treni hiyo itaunganisha uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Msalato na Mji wa Serikali, alisema. “Wakati wa kuijenga Dodoma umefika ikiwa ni utekelezaji wa ndoto ya Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere” aliongeza. Dhamira ya Serikali ni kuboresha na kuimarisha miundombinu ya usafirishaji kwa wananchi wa Dodoma.

Akiongelea miradi aliyoiwekea mawe ya msingi, Rais amesema kuwa ujenzi wa miradi hiyo unakwenda vizuri. Amesema kuwa ameweka jiwe la msingi katika ujenzi wa soko linalogharimu shilingi bilioni 14.649 na stendi kuu ya mabasi inayogharimu shilingi bilioni 24.033. “Shukrani Waziri Jafo kunialika kwenye shughuli hii ya maendeleo. Wana Dodoma mnapenda maendeleo". Vilevile, amewataka kutunza miundombinu inayoendelea kujengwa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Aidha, Rais Dkt. Magufuli amewataka wananchi wa Dodoma kujipanga na kuchangamkia fursa za Serikali kuhamia Dodoma. “Ombi langu kwa wanadodoma mjipange kufanya kazi, fursa zimepatikana. Fursa ya soko ipo. Mkichelewa wengine watakuja kuchukua fursa hizi nanyi mtabaki watazamaji“ amesisitiza Rais Dkt. Magufuli.

Akiongelea miongoni mwa sababu za kuhamishia Makao Makuu Dodoma, alisema kuwa ni kuondoa umasikini wa wana Dodoma. “Serikali imetimiza wajibu wake, suala la uchumi wa mtu mmoja mmoja ni jukumu la mtu mwenyewe. Lazima mfanye kazi” alisisitiza Rais Dkt. Magufuli.

Rais aliwapongeza wananchi wa Dodoma kwa kupata miradi mingi. ”Nawapongeza wana Dodoma, mkiongozwa na viongozi wenu, Mkuu wa Mkoa, Meya, Mkurugenzi wa Jiji kwa kupata miradi hii yote, ni miradi mingi. Pongezi pia kwa kufanya mabadiliko katika Jiji lenu. Ni Jiji hili tu lenye maendeleo mazuri…Mkurugenzi wa Jiji umenifanya niwaamini vijana kuwa wanaweza kufanya makubwa” alisisitiza.  

Baadhi ya Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Magufuli (hayupo pichani) alipokuwa akihutubia wananchi wa Dodoma kwenye Stendi Kuu ya Dodoma.


Rais Mhe. John Pombe Magufuli akiwaaga wananchi baada ya mkutano wa hadhara na wananchi wa Dodoma.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.