• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

JPM azindua barabara ya Tunduma - Laela - Sumbawanga

Imewekwa tarehe: October 6th, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amezindua barabara ya Tunduma - Laela - Sumbawanga yenye urefu wa kilometa 223.2 ambayo ni sehemu ya barabara kuu katika ushoroba wa magharibi unaonzia Tunduma - Mpanda - Kigoma - Nyakanazi wenye urefu wa kilometa 1,286.

Ujenzi wa barabara hiyo umegharimu shilingi Bilioni 373 na Milioni 949 kwa ufadhili wa  mfuko wa changamoto za milenia (MCC) na kukamilika  kwake kumesaidia kuinua shughuli za kiuchumi katika ukanda wa nyanda za juu kusini na ukanda wa magharibi, na pia kumeunganisha usafiri kati ya Tanzania na nchi jirani za Malawi, Zambia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Burundi, Rwanda na Uganda.

Akizungumza katika sherehe za uzinduzi wa barabara hiyo zilizofanyika katika Mji Mdogo wa Laela Wilayani Sumbawanga, Mhe. Rais Magufuli amewapongeza wananchi wa Mikoa yote inayonufaika na barabara hiyo na amewahakikishia kuwa Serikali inayo dhamira ya dhati ya kuhakikisha barabaa kuu zote za ukanda wa magharibi zinajengwa kwa kiwango cha lami.

Ameishukuru Marekani kupitia MCC kwa ufadhili wa mradi huo, Rais Mstaafu Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa mradi huo kutekelezwa katika kipindi chake na ameipongeza Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano pamoja na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) kwa usimamizi wa ujenzi wa barabara hiyo, na pia amewataka wananchi na watumiaji wa barabara hiyo kutunza miundombinu yake kwa kutochimba mchanga kando ya barabara na madaraja, kutomwaga mafuta barabarani na kutoiba alama za barabarani.

Katika mkutano huo, Mhe. Rais Magufuli ameelezea kuchukizwa na taarifa za kuchomwa moto mitambo ya umeme jua ya mradi wa maji wa Mji Mdogo wa Laela uliogharimu shilingi Bilioni 1.7 na ameagiza waliohusika kukamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Aidha, baada ya kupokea malalamiko dhidi ya mkandarasi Fally Enterprises Ltd aliyepatiwa zabuni ya kujenga mradi huo pamoja na miradi mingine ambayo inadaiwa kutofanya kazi kama ilivyotarajiwa licha ya fedha zake kulipwa , Mhe. Rais Magufuli ametoa siku 7 kwa vyombo vya dola kumkamata, kuchunguza na kumfikisha katika vyombo vya sheria, na pia ameagiza Wizara ya Maji kuwachunguza na kuwachukulia hatua za kisheria maafisa wote wa wizara waliohusika kumpa zabuni mkandarasi huyo.

Chanzo: Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.