• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Juhudi na nidhamu yatakiwa kwa washiriki wa mafunzo ya Jeshi la Akiba Dodoma

Imewekwa tarehe: September 11th, 2024

Na. Rahma Abdallah, MPUNGUZI

MKUU wa Wilaya ya Dodoma, Alhaji Jabir Shekimweri amewataka washiriki wa mafunzo ya Jeshi la Akiba kuwa na nidhamu ya hali ya juu kwa muda wote wa mafunzo na kuzingatia yote watakayo fundishwa ili kuwa kuwa askari mahili.

Hayo aliyasema wakati akifungua mafunzo ya 17 ya Jeshi la Akiba Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa michezo wa Shule ya Sekondari Mpungunzi iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Alhaj Shekimweri alisema kuwa wakufunzi wa mafunzo hayo wanauzoefu mkubwa utakaowasaidia kuimarika katika kozi mbalimbali za jeshi la akiba. “Niwaase mfuate maelekezo, mfuate mafunzo yote ya medani, mafunzo ya kitendaji, pia kuwa na nidhamu wakati wote wa mafunzo. Msingi mkubwa wa kazi za jeshi ni nidhamu. Huwezi kuwa askari kama huna nidhamu. Kwahiyo, mtapimwa viwango vyenu vya nidhamu” alisema Alhaj Shekimweri.

Pia aliongeza kwa kusema “tafsiri ya kwanza ya nidhamu ni kuheshimiana ninyi kwa ninyi, kuwaheshimu viongozi wenu wa kambi, kuwaheshimu viongozi wanaokuja kuwatembelea na kuwatia nguvu huku mkitambua kuwa yote mnayoyafanya ni chini ya mwamvuli wa jeshi la ulinzi na usalama wa nchi yetu”.

Sanjari na hayo aliwasisitiza kujitokeza na kushiriki katika uboreshaji wa taarifa kwenye daftari la mpira kura pamoja na kushiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika mwezi Novemba, 2024. “Hakikisheni mnahuisha taarifa zenu na kwa wale ambao walikuwa na umri mdogo katika uchaguzi uliopita na sasa wamefikia umri wa kushiriki mkajiandikishe. Ukiona una sifa za kuwa kiongozi, chukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali na wakati ukifika shiriki kumpigia kura kiongozi atakayekufaa” Alhaj Shekimweri alisisitiza.

Alihitimisha kwa kuwapongeza washiriki wa mafunzo kwa utayari wao na uzalendo na kuwatakia heri katika muda wote wa mafunzo. Aidha, aliwataka wakufunzi wa mafunzo hayo kuwaandaa kikamilifu washiriki hao ili wawe raia wema kwa nchi yao.

Akiwasilisha taarifa ya mafunzo hayo, SSGT. Lusajo Mwakanyamale, Kaimu Mshauri wa Jeshi la Akiba Wilaya ya Dodoma alisema kuwa washiriki wa mafunzo hayo wametoka tarafa ya Dodoma mjiji pamoja na Zuzu. Alisema baadhi yao ni walinzi kutoka makampuni binafsi na wengine ni kutoka kwenye mitaa wanayoishi kwa mujibu wa sheria. “Afande mgeni rasmi napenda kukuhakikishia kuwa mafunzo haya yatafikia viwango vinavyokubalika na jeshi la akiba na watakuwa tayari kulitumikia taifa. Mafunzo haya yatafanyika kwa majuma 18 (miezi 4)” alisema SSGT. Mwakanyamale.

Mafunzo ya Jeshi la Akiba Wilaya ya Dodoma ni mafunzo ya awamu ya 17 yakilenga kuwajengea washiriki utimamu wa mwili, ukakamavu, ujasiri na uzalendo kwa taifa lao kupitia masomo mbalimbali ikiwa ni pamoja na usalama wa raia, huduma ya kwanza, ramani, zimamoto, uhamiaji na elimu ya kupambana na rushwa, alisema SSGT. Mwakanyamale.

Kwa upande wake Lameck Mashaka, Mshiriki wa mafunzo hayo alisema kuwa uzalendo kwa nchi ndio msukumo uliomfanya kujitokeza na kupata mafunzo hayo. Aliahidi kuzingatia mafunzo hayo na kuyafanyia kazi mara baada ya kuhitimu. “Nashukuru kwa kupatiwa nafasi hii ya ushiriki kwenye haya mafunzo na imani yangu kubwa nitaimarika na kwenda kuitumikia nchi yangu kwa uzalendo” alisema Mashaka.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.