• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kamati ya Bunge yajipanga kuinua Kilimo Hifadhi

Imewekwa tarehe: January 18th, 2020

KAMATI ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, imeishauri Serikali kuweka kipaumbele kwenye kilimo hifadhi kisera na kisheria ili kulinda ardhi na kuwa na kilimo chenye tija.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mahamoud Mgimwa, alisema hayo jana katika kikao cha kamati na wadau wa kilimo kilichohusu mipango na mikakati ya kuendeleza kilimo hifadhi na matumizi ya zana bora za kilimo katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Katika kikao hicho, kamati hiyo ilikutana na Shirika la Kilimo Hifadhi Tanzania (CFU) na Mtandao wa Kilimo Hifadhi Barani Afrika (ACTN), ambao wanashauri wakulima kutumia mbinu stahiki za kilimo hifadhi na matumizi sahihi ya pembejeo.

Mgimwa pia alitaka kujua namna serikali ilivyowekeza katika kilimo hifadhi.

"Kilimo hifadhi kina tija na si ndogo kwanza mkulima anapata mazao ya kutosha lakini pia kubana matumizi kwa kuwa matumizi ya mbolea hayatakuwapo kwa kiasi kikubwa, kwa hiyo kuna tija na hata vyakula vitakavyopatikana vitakuwa vya asili," alisema.

Alieleza hali hiyo itamwezesha mkulima kuuza mazao yake bila kikwazo chochote.

"Kamati itahakikisha serikali wanalipa uzito suala la kilimo hifadhi kwa kuweka sera na sheria, hatuna sababu ya kulikwepa tuliweke watu walijadili," alisema.

Akichangia katika kikao hicho, Mbunge wa Hanang, Mary Nagu, alisema kilimo ndiyo sekta itakayowainua wakulima na awali wakulima wa jimbo lake waliamini kuhusu kilimo hifadhi lakini baadaye walihamasishwa kutumia mbolea za kisasa, hivyo wataalam wana wajibu wa kutoa elimu kwa kina kuhusu hilo.

"Tutawatoaje kwenye matumizi ya mbolea ya kisasa, ili waendelee kuwa na imani, kama mliwaambia mbolea ya kisasa ikitumika kwa muda mrefu inaharibu ardhi kabisa, leo tunawezaje kurudisha hili la kilimo hifadhi kwa wakulima ambapo awali walikuwa wanaamini," alisema.

Nagu alisema suala la kilimo hicho linapaswa kuwa endelevu ili kuwasaidia wakulima na kuwataka wataalamu watoe elimu ya kutosha ili kunusuru ardhi ya Tanzania.

Naye Mbunge wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo, alisema uharibifu mkubwa wa ardhi unafanywa na mbolea na mwamko wa kutumia mbolea ni mkubwa na kuwaomba wataalam kutoa elimu namna ya kurutubisha ardhi kupitia kilimo hicho.

Mbunge wa Singida Kaskazini, Justine Monko, alisema wataalamu wanashauri mahindi yalimwe na maharage yasiyoliwa ili kuchangia ardhi kupata rutuba lakini elimu zaidi inahitajika kwa wakulima imekuwa ni vigumu kuweka mchanganyiko huo.

Awali, akiwasilisha kwa kamati mada ya uzoefu wa kilimo hifadhi barani Afrika, Mtendaji Mkuu wa ACTN), Mhandisi Saidi Mkomwa, alisema kuna haja ya kubadili kilimo cha sasa kuwa kilimo hifadhi yatakayoendana na matumizi sahihi ya zana za kilimo.

Alisema kuna tatizo kubwa la kilimo cha Tanzania kuchakaza udongo na hivyo kuna haja ya kulinda mazingira kwa manufaa ya taifa na vizazi vijavyo.

Alibainisha kuwa kuna fursa nyingi zinazojitokeza kwa Tanzania kutokana na mabadiliko yaliyoanza kujitokeza ikiwamo watanzania wengi kuhamia mijini na kwamba ifikapo mwaka 2030 kutakuwa na watu milioni 35 mijini ambao watategemea kununua chakula.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.