• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kamati ya Fedha na Utawala wakipongeza Kikundi cha Vijana Airsurf

Imewekwa tarehe: October 23rd, 2023

Kamati ya Fedha na Utawala wamekipongeza Kikundi cha Vijana Airsurf kinachojishughulisha na utoaji wa huduma ya TEHAMA ambazo ni huduma ya internet nyumbani na ofisini, usimikaji wa mtandao wa kiambo(LAN), mtandao mpana (WAN) na usimikaji wa kamera za usalama.

Pongezi hizo walizitoa walipofanya ziara katika ofisi za mradi huo kwa lengo la kukagua namna kikundi hicho kinavyoendesha shughuli zake.

Diwani Joan Mazanda Mjumbe Kamati ya Fedha na Utawala alisema kuwa vijana wengi wamekuwa wakijishughulisha na biashara ambazo zimezoeleka masikioni mwa watu, ni nadra kukuta vijana wa rika kama lao wakijishughulisha na biashara ya utoaji huduma ya TEHAMA.

“Nawapongeza sana kwa kutumia taaluma yenu nakuja na mpango wa biashara kama hii. Niwaombe muelekeze nguvu zenu kwenye kujitanganza msiishie kwenye masoko tu, nendeni mbali zaidi nendeni mashuleni na kwenye Taasisi za vyuo wanachuo ndio wanaongoza kwa kutumia intaneti pia mnavyotangaza na kutoa huduma nzuri mnajitengenezea mabalozi wa huduma yenu” alisema Mazanda.

Kwaupande wa Diwani Neema Mwaluko, Mjumbe Kamati ya Fedha na Utawala aliwapongeza kwa uthubutu wa kufungua ofisi na kutumia mkopo waliopewa na halmashauri vizuri hivyo, kuwaomba wajikite katika kutatua changamoto za biashara yao ili waweze kurejesha mkopo waliokopa.

“Nawapongeza sana ninyi ni vijana wa kuigwa. Wapo wanaoomba mkopo lakini wanaishia kugawana hela hawatekelezi lile andiko waliloombea mkopo lakini ninyi mmekuwa waaminifu na imara, msikate tamaa hakuna biashara rahisi. Angalieni namna yakutatua changamoto zenu ili biashara yenu iweze kufanya vizuri muweze kurejesha mkopo wenu kwa wakati, mnaporejesha mnatengeneza mazingira yakuaminika kwa kikubwa zaidi” alisema Mwaluko.

Akisoma taarifa ya mradi, Anna Kasebena Mratibu wa Mradi wa Airsurf, alisema kuwa wanaishukuru Halmashauri ya Jiji la Dodoma kupitia mkopo wa asilimia 4 kwa vijana waliweza kupata fedha zilizosaidia katika kutanua wigo wa biashara yao.

Kikundi cha Airsurf kilianza kikiwa na wateja wawili tu, baada ya kupata mkopo tulifanikiwa kufikisha wateja 53 na kuanzisha mradi wa kutoa huduma ya mtandao ijulikanayo kama Airsurf-Hotspot katika eneo la Rehema Nchimbi Complex. Kikundi kinakabiliwa na changamoto ya uhaba wa fedha za kuendeshea mradi kutokana na gharama kubwa zilizopo katika vifaa na uendeshaji wa shughuli za ICT na kutokuwa na ofisi ya kukidhi viwango hivyo, kutoaminika na wateja na wengine kushindwa kabisa kufika ofisini.

Kikundi cha Airsurf ni kikundi cha vijana kilichopo Kata ya Tambukareli jijini Dodoma, kilianzishwa mwaka 2021 na kufanikiwa kupata mkopo wa asilimia 4 wa vijana mwaka 2022 wa kiasi cha shilingi milioni 15.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.