• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kamati ya Fedha yaagiza Shule ya Mbabala isaidiwe

Imewekwa tarehe: July 19th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

KAMATI ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeagiza shule ya msingi Mbabala iliyopo katika Kata ya Mbabala iingizwe kwenye shule zenye mahitaji maalum ili iweze kusaidiwa kuboresha miundombinu ya kufundishia na kujifunzia.

Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe alipoongoza kamati yake kutembelea na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule hiyo.

Prof. Mwamfupe alisema “hali ya shule siyo nzuri. Shule hii ina msongamano mkubwa wa wanafunzi ni vizuri iingizwe katika shule zenye mahitaji maalum ili iweze kusaidiwa haraka. Tumetaarifiwa kuwa kuna darasa lililoanza kujengwa lakini halikukamilika, ni vizuri darasa hilo likapewa fedha kulikamilisha na walimu waongezwe shuleni hapa ili kupunguza tatizo la uhaba wa walimu”.

Akiongelea mipaka ya shule hiyo, aliagiza shule hiyo ipimwe na kuwekewa alama za mipaka (beacon). Shule hii ikipimwa itaondoa uwezekano wa maeneo yake kuvamiwa na wananchi na kuendeleza shughuli za kibinadamu na kuathiri mwenendo wa kufundisha na kujifunza kwa wanafunzi.

Akisoma taarifa ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa, mwalimu mkuu wa shule ya msingi Mbabala, Mwalimu Ezra Nathanael alisema kuwa shule yake ilipokea fedha shilingi 40,000,000 zikiwa ni fedha za mapato ya ndani kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa. “Mradi umekamilika hatua zote isipokuwa uwekaji wa vigae kutokana na fedha kuisha. Changamoto katika kutekeleza mradi huu ni kupanda kwa gharama za vifaa vya ujenzi. Changamoto nyingine ni uhitaji mkubwa wa vyumba vya madarasa, ambapo mahitaji ni vyumba 24, vilivyopo ni saba na upungufu ni 17” alisema Mwalimu Nathanael.  

Shule ya Msingi Mbabala ina jumla ya wanafunzi 1,076 baadhi yao wakitembea zaidi ya kilometa tano kwenda shuleni ikiwa na walimu saba na upungufu wa walimu 17 kufikisha mahitaji ya walimu 24.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.