• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kamati ya Fedha yaridhishwa na ujenzi wa madarasa Mkonze

Imewekwa tarehe: July 19th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

KAMATI ya Fedha na Utawala imeridhishwa na ujenzi wa madarasa mawili katika shule ya sekondari Mkonze iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma kupitia mapato ya ndani.

Mjumbe wa Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Sospeter Mazengo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya alisema kuwa kazi ya ujenzi wa madarasa mawili ni nzuri na kuitaja kuwa inaonekana. “Tumekuja kuona na kukagua matumizi ya fedha na utekelezaji wa miundombinu ya madarasa katika shule hii. Lengo la ukaguzi huu ni kuona kwa macho na pale tunaposoma taarifa zenu na kuona zina mashiko tunazifanyia kazi na kutekeleza mapendekezo mnayotoa. Pale tunapozitilia shaka tunaagiza Mkaguzi wa Ndani kufanya ukaguzi katika eneo husika” alisema Mazengo.

Aliagiza ifanyike tathmini ili kupata makadirio halisi ya gharama ya ukamilishaji wa mradi huo. Vilevile, alishauri kuwa ukamilishaji wa mradi huo uwe kwenye vipaumbele vya mpango na bajeti wa kata.

Akisoma taarifa fupi ya utekelezaji wa mradi wa nyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkonze, Mkuu wa shule hiyo, Mwalimu Andrew Rumishaeli alisema kuwa shule yake ilipokea shilingi 40,000,000.

Mwalimu Rumishaeli akiongelea hatua ya utekelezaji wa mradi alisema kuwa mradi huo umetekezwa kwa asilimia 97. Alisema kuwa kazi zinazotarajia kufanyika ni usukaji wa umeme awamu ya pili na upachikaji wa vioo vya madarasa na shata za milango. “Changamoto katika utekelezaji wa mradi huu ni fedha kutotosheleza kwa ajili ya ukamilishaji wa mradi kwa asilimia 100 kwa sababu fedha kwa ajili ya vifaa vya umeme kwa awamu ya pili na shata za milango hazijatosha” alisema Mwalimu Rumishaeli.

Aidha, alisema kuwa ujenzi huo unahitaji fedha kidogo ili uweze kukamilika. Alikitaja kiasi cha fedha kinachohitajika kukamilisha ujenzi huo kuwa ni shilingi 2,400,000.

Wakati huohuo, mkuu huyo wa shule alikumbushia kukamilishwa kwa ujenzi wa jengo la utawala lililoanza kujengwa miaka miwili iliyopita. “Kuna jengo la utawala ilishapita miaka miwili ya fedha, tunaomba tusaidiwe kulikamilisha. Tulipewa shilingi 55,000,000 kwa ajili ya ujenzi wake, hadi sasa bado kama shilingi 45,000,000 ili likamilike. Kutokamilika kwa jengo hilo maana yake tunaendelea kutumia madarasa kwa shughuli za kiutawala. Jengo la utawala likikamilika litaachia madarasa yaendelee kutumika kwa madhumuni yaliyokusudiwa” alisema Mwalimu Rumishaeli.

Mwenyekiti Kamati ya Ujenzi wa shule hiyo, Mohamed Missanga alisema kuwa wakati wa utekelezaji wa ujenzi huo, wanazingatia kuwa vitakuja vizazi vingi kutumia madarasa hayo. “Tunawashukuru kwa kuja kututembelea na kutukagua, dhamira yetu ni ukamilishaji wa mradi, kuusimamia vizuri. Pongezi kwa mkuu wa shule na watendaji kwa kuwa karibu katika utekelezaji wa mradi huu” Missanga.

Shule ya sekondari Mkonze ina jumla ya wanafunzi 1,164, wasichana wakiwa 646 na wavulana 518, ikiwa na walimu 56. Shule hiyo inahudumia mitaa minane ya Kata ya Mkonze ambayo ni Chidachi, Miganga, Chinyika, Bwawani, Chisichiri, Muungano ‘A’, Muungano ‘B’ na Nzinje.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.